Tuesday, May 21, 2013
Monday, May 20, 2013
KAMPUNI YA MONTAGE YAIKABIDHI WAMA MILIONI 70 KUSAIDIA AFYA YA MAMA NA MTOTO TANZANIA
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Salma Kikwete (katikati) akisalimina na Mkurugenzi wa ITV, Joyce Mhavile na kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited, Teddy Mapunda.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA, Salma Kikwete (kulia) akizungumza na Uongozi wa Montage pamoja na wadhamini wa Harambee iliyoongozwa na Kampuni ya Montage kwaajili ya kuchangisha fedha kwaajili ya kusaidia matibabu ya Mama na Mtoto nchini Tanzania.

Mkurugenzi wa ITV, Joyce Mhavile (kushoto)akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited, Teddy Mapunda kabla ya kukabidhi hundi kwa Uongozi wa WAMA.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Salma Kikwete akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni 70 kutoka kwa Mkurugenzi wa Montage Limited, Teddy Mapunda ikiwa ni mchango wa kampuni hiyo katika kuchangia Afya ya Mama na Mtoto.
Fedha hizo ni sehemu ya michango ya wadau mbalimbali iliyopatikana katika harambee maalum iliyopendeshwa na Montage hivi karibuni. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Fedha wa Montage, Zainabu Mkindi (wapili kushoto)na kulia ni Katibu wa WAMA, Daud Nassib. Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki.
Mzee Ally Kleist Sykes Afariki Dunia Jijini Nairobi

FAMILIA YA SYKES INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MZEE WAO ALLY KLEIST SYKES (PICHANI) KILICHOTOKEA JANA MEI 19, 2013 KATIKA HOSPITALI YA AGA KHAN JIJINI NAIROBI, KENYA, ALIKOKUWA AMELAZWA.
MSIBA UKO NYUMBANI KWA MAREHEMU MBEZI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM. MWILI WA MAREHEMU ULITARAJIWA KUWASILI JIJINI USIKU USIKU WA KUAMKIA LEO.
MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA LEO MEI 20, 2013 KATIKA MAKABURI YA KISUTU BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUSWALIWA KATIKA MSIKITI WA KIPATA WAKATI WA SWALAT ALAASIR.
HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.
إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعونَ
Inna-na lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Hakika sisi sote ni waja wa Mwenyezi Mungu, na kwake tutarejea.
Surely we belong to Allah, and to Him shall we return
NA H@KI NGOWI
Abu Dhabi Airport installs world’s first GoSleep sleeping pods for travelers

With the jet-set lifestyle of most executives and other intercontinental travelers, the foremost luxury then is the much needed sleep. Since one’s schedules and engagements can not be changed, short power naps can be helpful to emerge rejuvenated and refreshed for busy times ahead.
For this reason, the idea of sleeping pods came into being, and they seemed to turn rather tech-loaded for the demands of these discerning travelers.
The Podtime sleeping pod and the Alberto Frias sleeping pod are the manifestations of these special demands. One place where one can now think of taking power-naps in such luxurious settings at a public space, is the Abu Dhabi International Airport (AUH) where there are have been 10 such GoSleep sleeping pods already installed in Terminal 1 and 3, and 35 are to arrive by next year.
Being one of the busiest airports in the Middle East, AUH needed such facilities for their premises where some travelers are flying across diverse geographical zones. Not just this, but by next year, one would see upgraded facilities of wi-fi internet, and charging slots for most personal devices in these GoSleep sleeping pods. Currently they are on hire for $12.12 (£8) to the hour.

The stylish Finish designed sleeping pods are easy to operate, where the user lies down, and shuts him/herself from any form of external disturbance like noise, or gathering crowds. On top of being able to catch up on some sleep between journeys, one could even be accessing the internet, charging personal devices, and even store their personal luggage in these pods.

Recently the Abu Dhabi had been conferred a 4-star Skytrax rating by the Airport Council International (CI), and this effort to gift the travellers some sleep at the airport, perhaps speaks of their efforts to go even further. Not many airports have this additional feature, but incase one is travelling in Russia, the Moscow Airport could be the place to notice such ‘sleeping corners’.
SOURCE: CLICK HERE
SOURCE: CLICK HERE
Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu katibu mkuu wa CHADEMA Taifa, Zitto Kabwe Afunika Tabora

Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu katibu mkuu wa CHADEMA taifa, Zitto Zuberi Kabwe akiunguruma mbele ya mamia ya wanachama wa Chadema Mjini Tabora Jana Wakati wa Uzinduzi wa matawi ya chama katika kila Kata ya Mji huo.
Wakati huo huo chadema kimefanya ufunguzi wa kampeni za uchaguzi wa vijiji katika jimbo la Naibu Katibu Mkuu wa CCM mwigulu nchemba Zilifunguliwa na Ally Bananga .Uchaguzi ni wa Vijiji 8 na Vitongoji 28.
Picha na Habari na Chadema
Dubai May Build New World’s Tallest Tower
By Mohamed Gabal
Dubai plans to build a new tower taller than Burj Khalifa and Kingdom Tower, said media reports quoting Mohammed Alabbar, Emaar Properties Chairman.
It is notable that, Burj Khalifa, built in October 2009, is set to be overtaken by Kingdom Tower which is under construction in KSA.
SOURCE: CLICK
It is notable that, Burj Khalifa, built in October 2009, is set to be overtaken by Kingdom Tower which is under construction in KSA.
SOURCE: CLICK
Kitimutimu cha Polisi na Wamachinga Iringa Jana, Mbunge wa iringa Mjini-Chadema Mch. Msigwa (Mb)Akamatwa
Mbunge
wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA)Picha juu amekamatwa na polisi jana hii kwa tuhuma kuwa ndiye chanzo cha kuhamasisha wafanya biashara
wadogo wadogo (wamachinga) kufanya vurugu huko Iringa.Askari
polisi wa kutuliza ghasia (FFU) katika Manispaa ya mji wa Iringa pia
imewakamata zaidi ya watu hamsini, akiwemoo aliyekuwa mgombea udiwani
katika kata ya Mvinjini, Abuu Majeck.
Biashara zilisimama wakati wa sekeseke hilo, moshi ulitanda kutokana na matairi kuchomwa moto katika barabara za kuu ya Iringa-Dodoma na ile ya Mashine Tatu. Jana hii pia, Mbunge huyo alikuwa katika eneo la chuo cha Tumaini kwenye harambee iliyokuwa imehudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye kama inavyoonekana kwenye pichaa chini

Mbunge wa iringa Mjini-Chadema Mchn Msigwa (kulia)akizungumza na msaidizi wa askofu wa KKKT dayosisi ya Iringa muda mfupi kabla ya kukamatwa na polisi jana
FFU WAPAMBANA NA WAMACHINGA IRINGA MJINI JANA
Mbunge wa jimbo la Iringa mjini-Chadema mchungaji Peter Msigwa akiwasili eneo la vurugu kabla ya kuanza kwa vurugu hizo
Mbunge wa Iringa Mjini-Chadema Mch Msigwa akiondoka eneo la mashine tatu
Wafanya Biashara Machinga wakisukuma gari ya mbunge wa iringa Mjini-Chadema Mch Msigwa
Askofu wa Kanisa Katoliki,Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo awatoa hofu waumini, ataka waendelee kusali

Askofu wa Kanisa Katoliki,Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.
****
Askofu wa Kanisa Katoliki,Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewataka waumini wa kanisa hilo kutoogopa kifo badala yake waendelee kwenda makanisani licha ya kuwapo kwa vitisho vya kushambuliwa.
Pengo alisema hayo jana katika Kanisa la Mtakatifu Joseph alipokuwa akitoa sakramenti ya kipaimara na aliwataka wasiwe na hofu lakini waendelee kumwamini Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu.
“Tuendelee kwenda makanisani,kamwe tusiogope kuuawa,tuwe na imani kwamba Yesu Kristo ndiye mlinzi wetu na ndiye atuongozaye,”alisema Pengo.
Kardinali Pengo alisema hata kama vyombo vya dola vitakuwa vimeshindwa kuwalinda,waumini kamwe wasiache kwenda makanisani kwa ajili ya kuabudu.Kwa Habari zaidi Bofya na Endelea.......
JK ALIPOTEMBELEA BANDA LA NSSF KATIKA KILELE CHA WIKI YA MIFUKO YA JAMII DODOMA
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkrugenzi Mkuu wa
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau wakati alipowasili kwenye maonesho ya Wiki ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii mjini Dodoma.
Rais Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Mkrugenzi Mkuu wa
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk Ramadhan Dau alipotembelea banda la NSSF wakati wa kufunga
maonesho ya Wiki ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyomalizika mwishoni mwa wiki
mjini Dodoma. Wa pili kushoto ni Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka. (Na
Mpiga Picha Wetu)
Rais Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifandji ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori wakati alipotembelea banda la NSSF katika maonesho ya Wiki ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyofanyika mjini Dodoma

Rais Jakaya kikwete akikaribishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shiorika la taifa la hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhani Dau alipowasili katika banda la NSSF. Kulia ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifandji ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori.

Mh. Rais Jakaya Kikwete akisoma jarida linaloonyesha kazi za NSSF.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau akifafanua jambo wakati wa mahojiano na waandishi wa habari.
HABARI NA ANKAL ISSA MICHUZI
HABARI NA ANKAL ISSA MICHUZI
The Big Boss Wa Benchmark Production Inayoratibu Shindano La Bongo Star Search, Rita Poulsen ‘Madam’ Apata Ajali Mbaya Ya Gari.

Rita Poulsen ‘Madam’.
Na Imelda Mtema
KILICHOMPATA Madam Rita kinasikitisha! Ndivyo unavyoweza kusema ukibahatika kumuona the big boss wa Benchmark Production inayoratibu Shindano la Bongo Star Search, Rita Poulsen ‘Madam’ anayetembelea magongo baada ya kupata ajali mbaya ya gari.
Rita Poulsen ‘Madam’.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda baada ya kuwa kimya muda mrefu ikielezwa kuwa alipata ajali hiyo kitambo, Madam Rita alisema kuwa kwanza kabisa anamshukuru Mungu kwani anaamini kila kitu kinachotokea chini ya jua kina sababu yake na hata alipopata ajali hiyo alimshukuru kwa kutoka salama.
Madam Rita aliendelea kueleza kuwa ajali hiyo aliipata katikati ya Jiji la Dar na kusababisha kuvunjika kwa kifundo ‘enka’ cha mguu wa kulia hivyo kumsababishia kutembelea magongo baada ya hospitali kumuwekea ‘hogo’.
“Namshukuru Mungu kwanza kwa kunitoa salama katika ile ajali japokuwa sijapona vizuri,” alisema Madam Rita.
Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kuwa alipopata ajali hiyo alikimbizwa katika Hospitali ya Muhimbili kwenye Taasisi ya Mifupa ya Moi lakini hali ilipokuwa kuwa mbaya alihamia katika hospitali moja ya Kichina ambapo kwa sasa amepata nafuu.
HABARI NA GPL
DIAMOND, NEY WA MITEGO WAFANYA KUFURU DAR LIVE
Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.Sunday, May 19, 2013
YANGA YAIGONGA SIMBA 2-0, Yatwaa kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara Jana

Nahodha wa Yanga, Nidir Haroub 'Canavaro' akiwa amenyanyua kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara pamoja na wachezaji wenzakeya Simba SC.
****
Timu ya Yanga jana imewaadhibu watani wao wa jadi, Simba SC baada ya kuwalaza kwa bao 2-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mabao ya Yanga yamefungwa na Didier Kavumbagu na Hamis Kiiza. Baada ya mchezo huo, Yanga SC ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara Jana
Saturday, May 18, 2013
Rasimu ya Sera ya Gesi Asilia aionavyo Mhe Zitto Kabwe

Nimepata muda kidogo wa kuipitia hii rasimu ya 3 nikiwa safarini kwenda Tabora kwa shughuli za chama changu cha CHADEMA , nina maoni ya awali kama ifuatavyo;
1). Kwa ujumla kupata Sera mpya ya gesi asilia ni hatua muafaka japo imechelewa sana. Hata hivyo ni bora kuchelewa kuliko kutofika kabisa. Ni vema wananchi wachukue fursa hii kuisoma na kuijadili rasimu hii na kuiboresha ili iwezeshe wananchi wenyewe kufaidika na utajiri ambao nchi yetu imejaaliwa.
2). Sera ina jumla ya sura Sita. Sura ya kwanza ya inaweka sababu na masuala ya jumla na utangulizi . Sura ya pili inaweka sababu za kuwepo kwa sera mpya na madhumuni maalumu, Sura ya tatu ndio yenye matamko ya msingi ya kisera (fundamental policy issues) ikiwemo masuala ya miundombinu ya gesi kwa ajili ya soko la ndani, usimamizi wa mapato yatokanayo na gesi asilia na masuala ya ‘’ local content’’. Sura hii pia imezungumzia masuala ya uwazi na uwajibikaji. Sura ya nne ni masuala ya mfumo wa kisheria na udhibiti na sura ya tano ni taasisi za usimamizi wa sera ya gesi asilia. Sura ya sita ni hitimisho. Kila sura imeweka matamko ya kisera.
3). Rasimu ya sera imeshindwa kutofautisha suala la Mafuta na Gesi kuwa ni suala la Muungano au sio suala la muungano katika muktadha wa Katiba mpya inayojadiliwa sasa. Hii inadhihirisha umuhimu wa kuwianisha mchakato wa katiba na michakato mingine inayoendelea nchini. Hivi sasa Zanzibar inajiandaa kuwa na sera na sheria yao ya mafuta ya gesi, iweje sera hii itamke gesi asilia ni mali ya Jamhuri ya Muungano wakati upande mmoja wa Muungano utakuwa unafaidi utajiri wake peke yake? Rasimu ya sera imeshindwa kutambua kuwa kuna vitalu vya mafuta na gesi ya (vitalu namba 9-12) vimesimamisha shughuli kwa sababu Serikali ya Zanziabar haitambui mafuta na gesi kuwa suala la muungano. Rasimu inapaswa kuzingatia jambo hili kabla ya kupata sera yenyewe.
4). Rasimu imetamka katika ukurasa wa 9 kwamba sera hii haitambui shughuli za utafutaji (‘This policy document only covers mid-and downstream segments’ ndio nukuu ya neno kwa neon ya Sera hii). Hiki ni kichekesho cha milenia .
Taifa linawezaje kuandika sera ya gesi asilia kwa upande wa uchuuzi tu (biashara) na kuacha kazi yenyewe haswa ya utafutaji na uchimbaji (exploration and exploitation are upstream). Shughuli za utafutaji na uchimbaji ndio msingi haswa wa sera ya gesi asilia.
Mikataba yote huamuliwa kwa kuzingatia kwanza utafutaji, shughuli nyingine ni biashara tu ya kitakachogunduliwa . Rasimu kuacha kabisa eneo la utafutaji na uendelezaji (upstream) ni sawa na kutokuwa na sera kabisa.
Kwa namna eneo hili lilivyoachwa kuna harufu ya mkakati wa siri wa kuwanyima wananchi msimamo wa kisera kuhusu utajiri wao unavyonyonywa . Sentensi hii yenye maneno 10 katika uk. wa 9 wa kijitabu cha rasimu ya sera unaondoa kabisa umuhimu wa sera yenyewe wakati dhumuni kuu la sera linatamkwa uk.6 kwamba Gesi asilia ni mali ya wananchi wa ‘Jamhuri ya Muungano’ wa Tanzania’’ kurasa tatu baadaye zinaiondoa sera kwenye eneo hilo la umiliki wa mali hii ( Upstream). Tumeamua kuandika sera ya uchuuzi wa gesi asilia?
5). Rasimu katika 3.2.2(uk.24) imeweka matamko ya kisera kuhusu uwazi na uwajibikaji . Uwazi ndio eneo ambalo watanzania wengi walikuwa wanasubiri kwa hamu sana . Usiri wa mikataba katika sekta mbali mbali nchini ni chanzo cha ufisadi na uporaji wa utajiri wa mali yetu. Sera hii imeJibu swala hili? HAPANA. Sera haisemi ni namna gani mikataba itakuwa wazi kwa wananchi. Sera haisemi ni namna gani wananchi wataiwajibisha Serikali na vyombo vyake (Accountability) kwenye masuala ya mafuta na gesi. Sera imepiga porojo kuhusu uwazi na uwajibikaji. Bila misingi imara ya Uwazi na Uwajibikaji katika rasilimali ya gesi asilia, sera haina maana yoyote ile.
6). Serikali ni lazima ijue kwamba hivi sasa nchi yetu nchi tajiri yenye watu masikini.[i] sera ya gesi inapaswa kutuondoa kuwa nchi yenye laana ya rasilimali. Sera hii haina mwelekeo huo kabisa . Sera inapaswa kuwezesha wananchi kupata thamani ya maliasili yetu na kuwezesha matumizi mazuri ya mapato yatokanayo na utajiri wa nchi.
Sera yetu lazima ioneshe dhahiri kwamba gesi asilia ni mali ya wananchi na uendelezaji na unyonyaji wa rasilimali hii utafaidisha wananchi kwanza na kwa ruhusa yao (Prior informed Consent Principle) sera ni lazima itamke hilo kinagaubaga.Sera ni lazima ionyeshe kuwa katika ushindani wa soko makampuni ya mafuta na gesi asilia yatapata faida ya halali ( normal retuns) ya uwekezaji wao na kwamba lolote linalozidi litabakia kuwa mali ya wananchi wa Tanzania.
Mkakati wa makampuni ya mafuta na gesi asilia ni kuhakikisha taifa linapata kiduchu na wanasaidia serikali kutoa majibu ya kipato hicho kiduchu. Watanzania hawatakubali tena.
7). Ni lazima tuseme kuwa tunataka utajiri wetu uwe neema kwa wananchi wetu, na siyo laana. Maendeleo yetu yatategemea ni namna gani tunafaidika na utajiri wetu wa maliasili kama gesi asilia. Sera ya Gesi Asilia itujengee imani hiyo. Hii Sera (Rasimu) inapaswa iangaliwe upya na hasa maeneo ya uwazi na uwajibikaji.
Kabwe Z. Zitto, Mb Kigoma Kaskazini
Tabora, tarehe 18 Mei 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)
