SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, July 11, 2016

KILIMANJARO COOPERATIVE BANK (KCBL) YASHEREHEKEA MIAKA 20 TANGU KUANZISHWA KWAKE

Matembezi yakipita katika mzunguko wa YMCA kuekea katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika.
Baadhi ya wageni wakichukua taswira ya matembezi hayo mara baada ya kupita barabara ya Rau katika manispaa ya Moshi.
Brass Band ya Chuo cha Polisi Moshi ikiongoza matembezi ya Hisani ikiwa ni sehemu mojawapo ya kusherehekea miaka 20 ya Benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (KCBL) .
Baadhi ya wananchi katika mji wa Moshi wakishiriki matembezi hayo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Executive Solution ambayo imeratibu sherehe hizo akiongoza njia ya matembezi hayo ndani ya uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika.
Brass Band ya Chuo cha Polisi Moshi ikiingia katika uwanja wa Chuo kIkuu cha Ushirika Moshi.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) Prof Faustine Bee akifurahia jambo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadick wakati wakijiandaa kupokea maandamano hayo.katikati ni Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Meck Sadick (kulia) akizungumza jambo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) wakati wakiongojea maandamano hayo ,katikati ni Mkuu Mpya wa wilaya ya Moshi, Kipi Warioba.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadick akipokea maandamano ya wana Ushirika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi ,
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadick akizungumza mara baada ya kupokea maandamano ya wanaushirika ikiwa ni sehemu ya kusherehekea miaka 20 ya Kilimanjaro Cooperative Bank (KCBL).
Meza Kuu.
Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Kipi Warioba akizungumza wakati wa sherehe hizo zilizofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki ya Ushirika Kilimanjaro (KCBL) Reginald Hosea akizungumza mara baada ya maandamano kuwasili katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.
Meneja Mkuu wa Benki ya Ushirika Kilimanjaro (KCBL) Elizabeth Makwabe akizungumza katika sherehe za kutimiza miaka 20 ya benki hiyo .
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Prof Faustine Bee akizungumza katika sherehe hizo zilizofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog Kanda ya Kaskazini.

0 comments:

Post a Comment