SHINDANO LA KUTAFUTA WIMBO WA YANGA KUPITIA RADIO CLOUDS FM
Dawati la habari za michezo na burudani Clouds Fm.
Mmoja kati ya watangazji maarufu wa radio Clouds Fm Bw Ephraim kibonde
Uongozi wa Mabingwa wa Soka nchini Yanga ya jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na Kampuni ya Clouds Media kupitia radio yake ya Clouds kwa pamoja wamezindua shindano la kutafuta wimbo maalumu wa Klabu ya Yanga utakaoshindaniwa na Wasanii mbalimbali hapa nchini ambao wimbo huo utakapopatikana utatumika katika mashindano mbalimbali pamoja na shughuli za klabu hiyo.
Taarifa hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam hii leo na Ally Mayayi ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Klabu ya Yanga ambaye pia ni mjumbe wa Kamati inayosimamia zoezi zima la upatikanaji wa wimbo maalum wa Klabu hiyo.
Mayayi amesema uzinduzi huo umefanyika Januari 29 Mwaka huu jijini Dar es Salaam na unatarajiwa kukamilika Februari 7 Mwaka huu.Katika kufanikisha zoezi hilo linafanikiwa jumla ya nyimbo kumi bora zitachaguliwa na wanachama wa Klabu hiyo kwa aajili ya kupata wimbo mmoja ambao utakuwa ni mahususi utakaotumika katika mambo mbalimbali ikiwemo michuano ya ndani nchi pamoja na ya kimataifa ikiwemo shughuli za Kimaendeleo za Klabu ya Yanga. alisema Mayayi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo mara baada ya kupatikana kwa wimbo huo maalum Msanii na wimbo huo utatangazwa katika sherehe za Yanga Day zinazotarajiwa kufanyika Februari 12 Mwaka huu jijini Dar es Salaam na mshindi aliyepatikana anatarajiwa kukabidhiwa zawadi yake.
Klabu ya Yanga moja ya Klabu Kongwe hapa nchini hivi karibuni ilianzisha Kampeni ya kutafuta wimbo maalum kama kitambulisho kwa wapenzi na wanachama wa Klabu hiyo. Wimbo pekee ambao ulikuwa ukitumika katika shughuli mbalimbali zinazohusu klabu ya Yanga ni ule uliotungwa na Mwanamuziki Pepe Kalle Yanga Africa Mabingwa wa soka wa Afrika Mashariki na Kati ambao unatumika katika vituo mbalimbali vya radio hapa nchini.
Afisa Habari - Young Africans Sports Club ( YANGA)
**********************
TENGA ACHAGULIWA TENA CECAFA
Leodgar Tenga.


Taifa Stars yarejea nyumbani baada ya kuadhibu Chad 2-1
Kocha wa timu ya taifa Taifa Stars Jan Paulsen akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo, mara baada ya timu hiyo kuwasili ikitokea N'Djamena nchini Chad, ambako ilicheza na timu ya taifa ya nchi hiyo na kuifunga magoli 2 kwa 0. Timu hizo zitarudiana siku ya jumanne wiki hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Taifa Stars inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili kuingia katika hatua ya makundi kwa ajili ya kinyang'anyiro cha kushiriki kombe la dunia mwaka 2014 nchini nchini Brazil.