ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A LOWEST COST AND ALSO SEND TO US NEWS, EVENTS FOR MORE INFORMATION CONTACT US TELEPHONE: +919160901191 E-mail: ally.shaaban@yahoo.com | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU NA PIA TUTUMIE HABARI, MATUKIO KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI KWA SIMU: +919160901191 Barua Pepe: ally.shaaban@yahoo.com | DO YOU NEED TO CREATE BLOG CONTACT US HERE | UNAHITAJI KUFUNGUA BLOG WASILIANA NASI HAPA

SPORTS

SHINDANO LA KUTAFUTA WIMBO WA YANGA KUPITIA RADIO CLOUDS FM
Dawati la habari za michezo na burudani Clouds Fm.
Mmoja kati ya watangazji maarufu wa radio Clouds Fm Bw Ephraim kibonde
Uongozi wa Mabingwa wa Soka nchini Yanga ya jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na Kampuni ya Clouds Media kupitia radio yake ya Clouds kwa pamoja wamezindua shindano la kutafuta wimbo maalumu wa Klabu ya Yanga utakaoshindaniwa na Wasanii mbalimbali hapa nchini ambao wimbo huo utakapopatikana utatumika katika mashindano mbalimbali pamoja na shughuli za klabu hiyo.
Taarifa hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam hii leo na Ally Mayayi ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Klabu ya Yanga ambaye pia ni mjumbe wa Kamati inayosimamia zoezi zima la upatikanaji wa wimbo maalum wa Klabu hiyo.
Mayayi amesema uzinduzi huo umefanyika Januari 29 Mwaka huu jijini Dar es Salaam na unatarajiwa kukamilika Februari 7 Mwaka huu.Katika kufanikisha zoezi hilo linafanikiwa jumla ya nyimbo kumi bora zitachaguliwa na wanachama wa Klabu hiyo kwa aajili ya kupata wimbo mmoja ambao utakuwa ni mahususi utakaotumika katika mambo mbalimbali ikiwemo michuano ya ndani nchi pamoja na ya kimataifa ikiwemo shughuli za Kimaendeleo za Klabu ya Yanga. alisema Mayayi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo mara baada ya kupatikana kwa wimbo huo maalum Msanii na wimbo huo utatangazwa katika sherehe za Yanga Day zinazotarajiwa kufanyika Februari 12 Mwaka huu jijini Dar es Salaam na mshindi aliyepatikana anatarajiwa kukabidhiwa zawadi yake.
Klabu ya Yanga moja ya Klabu Kongwe hapa nchini hivi karibuni ilianzisha Kampeni ya kutafuta wimbo maalum kama kitambulisho kwa wapenzi na wanachama wa Klabu hiyo. Wimbo pekee ambao ulikuwa ukitumika katika shughuli mbalimbali zinazohusu klabu ya Yanga ni ule uliotungwa na Mwanamuziki Pepe Kalle Yanga Africa Mabingwa wa soka wa Afrika Mashariki na Kati ambao unatumika katika vituo mbalimbali vya radio hapa nchini.
Afisa Habari - Young Africans Sports Club ( YANGA)

**********************
TENGA ACHAGULIWA TENA CECAFA
 
Leodgar Tenga.
***********
Taifa Stars yarejea nyumbani baada ya kuadhibu Chad 2-1
Kocha wa timu ya taifa Taifa Stars Jan Paulsen akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo, mara baada ya timu hiyo kuwasili ikitokea N'Djamena nchini Chad, ambako ilicheza na timu ya taifa ya nchi hiyo na kuifunga magoli 2 kwa 0. Timu hizo zitarudiana siku ya jumanne wiki hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Taifa Stars inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili kuingia katika hatua ya makundi kwa ajili ya kinyang'anyiro cha kushiriki kombe la dunia mwaka 2014 nchini nchini Brazil. 
Kulia ni Mchezaji wa Taifa Stars Nizar Khalfan na kushoto ni Henry Joseph wakiongoza wenzao wakati walipowasili kwenye uwanja wa ndege wa mwalimu J.K.Nyerere leo jijini Dar es laam wakitokea nchini Chad.
Kocha wa timu ya taifa Taifa Stars Jan Paulsen akiingia kwenye basi la timu hiyo, mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere DIA jijini Dar es salaam.
Golikipa watimu ya taifa Juma K. Juma akiwa katika pozi katika basi la Taifa Stars leo.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweriers (SBL) Teddy Mapunda na Meneja wa kinywaji cha Serengeti Lager Allan Chonjo kushoto, wakiwapongeza wachezaji wa Taifa Stars, mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo alasiri.
Mwandishi wa habari wa BBC nchini David Eric Nampesya akimhoji katibu mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Angetile Osiah wakati wa mapokezi ya Taifa Stars iliyowasili nchini leo ikitokea nchini Chad.
Mwandishi wa habari wa BBC nchini David Eric Nampesya akipozi kwa picha na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweriers (SBL) Teddy Mapunda.
Mzungu huyu ambaye hakufahamika jina lake mara moja, akipata taswira baada ya kuvutiwa na vijana hawa wanaofanya kazi ya promosheni ya bia ya Serengeti Lager.
Wachezaji hawa wa kesho nao wameshiriki kuwapokea kaka zao Taifa Stars wakati walipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo.
Mashabiki mbalimbali wamejitokeza kuja kuwapokea wachezaji wa timu yao Taifa Stars ilipowasili leo ikitokea nchini Chad. 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
KUSOMA HABARI ZILIZOPITA BOFYA NENO OLDER POSTS HAPO JUU ASANTE SANA KWA KUTEMBELEA NA KARIBU TENA