SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, January 5, 2015

AISEEE...HII NI KALI, ETI 2014,ULIFANYA NINI?? 2015 UTAFANYA NINI...ZINDUKA SOMA HAPA JITATHMINI UFIKIE NDOTO ZAKO


Ni kama juzi tu tuliposhangilia kuanza kwa mwaka mpya 2014. Wakati mwaka huu unaanza ulikuwa na shauku kubwa, ulijipangia mipango mikubwa na ulisema 'mwaka huu 2014 ni mwaka wangu'. Ikaisha Januari na kuanza Februari ilipofika Mei hukuwa na kumbukumbu yoyote kuhusu mambo yale uliyojiahidi wakati ukisherekea mwaka mpya. Na sasa mwaka umeisha tena, umeanza mwaka 2015, utajiwekea malengo makubwa na kusema huo ni mwaka wako!
Umekuwa unarudia utaratibu huu kila mwaka na bado hujastuka muda ambao unapoteza kadiri miaka inavyozidi kwenda. Leo nataka kwa pamoja tuende hatua kwa hatua jinsi ambavyo unaweza kuutumia vizuri mwaka huu 2015. Tunachokwenda kujadili hapa kitakuhitaji wewe kuwa makini na kukifanya ili uweze kubadili maisha yako.

Unapoanza mwaka 2015, tenga muda usiopungua saa moja. Katika muda huo kaa sehemu ambayo ni tulivu na hutopata usumbufu wowote. Zima simu yako/zako na kukaa wewe kama wewe. Katika muda huo sahau kuhusu matatizo yanayoendelea kwenye maisha yako, sahau kuhusu watu wanaokudai au unaowadai na hapa baki na nafsi yako tu. Katika muda huu kuwa na kitabu chako cha kuandika mipango yako na kalamu. Utakachokifanya hapa ni wewe kutafakari maisha yako yalipotoka, yalipo sasa na yanakoelekea.
 
Umetoka wapi?
Katika ukurasa mmoja wa kitabu chako andika kichwa cha habari, 'nimetoka wapi?' Katika ukurasa huu andika mambo yote yaliyotokea kwenye maisha yako kwa siku za nyuma. Andika ndoto zako zote ulizokuwa nazo tangu ukiwa mtoto, ukiwa shuleni na hata ulipokuwa unaanza kufanya kazi. Andika ni jinsi gani ulikuwa unafikiria maisha yako yatakuwa baada ya kipindi fulani. Pia tumia nafasi hii kuandika matukio makubwa yaliyotokea kwenye maisha yako na ambayo yamebadili sana maisha yako.

Katika sehemu hii andika maamuzi ambayo umewahi kufanya kwenye maisha yako na yakakuletea mafanikio makubwa. Na pia andika maamuzi ambayo umewahi kufanya na ukawa umekosea sana, yaani yakakufanya upoteze au uingie kwenye matatizo.

Wakati unaandika mambo haya usitoe hukumu yoyote, yaandike kama yalivyo na baadae utajua ni jinsi gani ya kutumia mambo haya.

Uko wapi sasa?
Baada ya kuandika ni wapi ulipotoka, fungua ukurasa mwingine na juu andika 'nilipo sasa'. Katika ukurasa huu andika mambo yanayoendelea sasa kwenye maisha yako. Andika ni kazi au biashara gani unafanya. Andika ni familia gani unaishi nayo. Andika ni kipato gani unapata sasa na pia andika changamoto gani unazopitia sasa.

Andika ni hofu gani unaipata kila siku na inatokana na nini. Andika pia kama kazi au biashara unayofanya unaipenda au inakusukuma kufanya makubwa zaidi kwenye maisha yako.

Ninaposema andika, namaanisha utafakari kisha uandike kile ulichotafakari. Pia kuwa mwaminifu sana na zoezi hili, usijaribu kujidanganya mwenyewe. Hakuna yeyote atakayeona ulichoandika hivyo andika ukweli wako wote.

Unaelekea wapi?
Hii ni hatua ya mwisho ya kuyaelewa maisha yako ili uweze kuchukua hatua sahihi. Katika hatua hii fungua ukurasa mwingine kwenye kitabu chako na kisha andika ninaelekea wapi? Katika ukurasa huu andika vitu vyote ambavyo unataka vitokee kwenye maisha yako. Andika ni kazi gani unataka kufanya na katika ngazi gani, kama ni biashara andika ni biashara gani unataka kufanya na unataka kuifanya kwa kiwango gani. Andika ni jinsi gani unayaona maisha yako miaka mitano ijayo, kumi ijayo na hata ishirini ijayo?

Jiulize kama ungepata nafasi ya kubadili maisha yako, ni maeneo gani hasa ambayo ungeyabadili. Jiulize kama ungejua kwamba huwezi kushindwa ni kitu gani ambacho ungekifanya? Na pia jiulize kama fedha isingekuwa tatizo kwako ni kazi au biashara gani ambayo ungeifanya?

Tafakari kwa kina kuhusu maisha yako na unataka yaelekee wapi. Andika chochote ambacho unafikiria au unataka kitokee kwenye maisha yako.

Mpango mkakati
Baada ya kujua umetoka wapi, uko wapi na unaelekea wapi sasa ni muda wa kuja na mpango mkakati wa maisha yako.
Kwa kuangalia ulipotoka angalia ni makosa gani uliyofanya na kisha jifunze kutokana na makosa hayo. Baada ya kujua ni kipi umejifunza usiendelee kurudia rudia tena makosa hayo. Pia angalia ni mambo gani uliyofanya yakakuletea mafanikio na angalia ni jinsi gani unaweza kufanya tena ili kupata matokeo bora zaidi.

Kwa kuangalia ulipo amua kwamba hutaendelea kama ulivyo sasa. Tambua kwamba unahitaji kufanya mabadiliko ili maisha yako yaweze kuwa bora zaidi. Angalia ni mambo gani unayofanya ambayo yanakupotezea muda na hayakusaidii kufikia malengo yako kwenye maisha.
Baada ya kuangalia sehemu hizi mbili, ulipotoka na ulipo sasa ni muda wa wewe kupanga vizuri kule unakotaka kufika. Kwa kuwa umeshajua ni wapi unataka kufika na ni jinsi gani unataka maisha yako yawe, sasa weka malengo yako. Unapoweka malengo weka ya muda mfupi na ya muda mrefu. Na pia weka mipango ya kutekeleza malengo hayo.

Mambo muhimu ya kuzingatia wakati unaweka malengo yako

Jinsi unavyoweka malengo ina athari kwenye kufikia malengo yako. Kama utaweka tu malengo kwa sababu kila mtu anasema mwaka huu nafanya hiki au kile basi utajikuta unashindwa kufikia malengo hayo. Yafuatayo ni mambo muhimu unayotakiwa kuzingatia wakati unaweka malengo yako;

1. Andika malengo yako
Moja ya kosa ambalo watu wengi huwa wanafanya wakati wa kuweka malengo ni kusema tu na kuishia hapo. Unatakiwa uandike malengo yako ili kuweka msisitizo zaidi. Unapoandika malengo yako inakufanya ufikiri zaidi na hivyo kuyapa uzito. Ila ukisema tu nataka kuwa na biashara kubwa na kuishia hapo hakuna chochote kitakachokusukuma kufikia lengo hilo.

2. Andika malengo kwenye maeneo yote muhimu kwenye maisha yako
Mara nyingi watu wanaposikia kuweka malengo wanafikiri unaweka malengo ya kazi, fedha au biashara. Kila eneo la maisha yako linatakiwa kuwekewa malengo. Hivyo unahitaji kuweka malengo ya kazi au biashara, weka malengo ya fedha, weka malengo ya mahusiano, weka malengo binafsi na pia weka maelengo ya kiafya. Ili kuwa na maisha yenye mlinganyo unahitaji kuwa na malengo katika maeneo haya muhimu kwenye maisha yako.

3. Weka utaratibu wa kupima malengo yako
Baada ya kuweka malengo na mipango ya maisha yako ya baadae ni muhimu kuwa na utaratibu wa kuweza kupima malengo yako. Ni muhimu uweze kupima kama upo kwenye njia sahihi ya kukufikisha kwenye malengo yako au umeshapotea njia. Ukikosa utaratibu wa kujipima utakuja kustuka mwaka mwingine umeisha na hujafanya jambo lolote la maana.

Ni muhimu sana kwako kufanya zoezi hili la kutathmini maisha yako. Unaweza kuona huwezi kupoteza muda kufanya haya tuliyojadili hapa, ila unapoteza muda mwingi sana kwa kufanya mambo ambayo hujui kama yanakufikisha kwenye malengo yako maishani. Muda unaotumia kupanga unaokoa muda ambao ungepoteza kwa kufanya jambo bila ya kupanga. Umemaliza mwaka 2014 kwa kujua ni wapi ulipokosea na wapi ulipofanya vizuri katika miaka yote iliyopita na anza mwaka 2015 ukiwa na mtazamo mpya wa kuleta mabadiliko ya kweli kwenye maisha yako.
Cha kujiuliza kikubwa,je hayo maisha unayoishi leo ndiyo ilikuwa ndoto yako ??
Mfano sasa hivi kuna mbinu nyingi za kufanya ili ubadili maisha yako...jiulize kama kuna walionza kwa kufanya biashara na Forever Living na mtaji wa 375,000/= na leo wanaingiza zaidi ya Tsh milioni 15 kila mmoja na wanamiliki magari ya kifahari,mapya na ya kisasa kama Ford Ranger,Land Rover Discovery4,Jeep Cherokee (U.S)Edition ya 2013,kwa nini wewe usifanye??Na unaposema biashara hii hauwezi,je hyo unayoiweza imekufanyia nini?kumbuka mwaka 2015 uwe karibu sana na watu waliofanikiwa,hao watakuongezea chachu ya kufikia ndoto zako...ila ukikaa karibu na walioshindwa hao watakusaidia kuangamiza ndoto zako..kumbuka mafanikio au kushindwa kwako kupo mikononi mwako na hulazimishwi...
Chukua Hatua, Kama umefurahishwa na ujumbe huu,
Tupigie simu +255 783 149 561 Tukushauri cha kufanya,..ni bure..

Tunakutakia Heri Ya Mwaka Mpya 2015 Wenye Mafanikio Tele!

0 comments:

Post a Comment