SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, September 26, 2011

Prof. Wangari Maathai Afariki Dunia

Prof Wangari Maathai
By Odhiambo Joseph, BBC, Nairobi
Mtunukiwa wa tuzo ya Amani ya Nobel Prof Wangari Maathai ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 71.
Mwanaharakati huyo mashuhuri wa mazingira na haki za binadamu wa Kenya Profesa Wangari Maathai amefariki dunia mjini Nairobi usiku wa kuamkia , Jumatatu kutokana na maradhi ya saratani.
Prof Karanja Njoroge ambaye ni mkurugenzi wa Green Belt Movement, shirika ambalo Prof Maathai alilianzisha amethibitisha kifo hicho.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari Prof Njoroge amesema wakati wa kifo chake Wangari alikuwa na wanafamilia na marafiki.
Marehemu ameacha watoto watatu, wawili wakiume na mmoja wa kike.
Profesa Wangari Maathai alipata tuzo la amani ya Nobel mwaka 2004, kufuatia juhudi za kupigania uhifadhi wa mazingira nchini Kenya.
Mbali ya kuwa Mwanaharakati wa Maswala ya Mazingira na haki za binadamu , Wangari Maathai pia alikuwa mwanasiasa shupavu. Amewahi kuhudumu kama Mbunge na Naibu waziri wa Mazingira nchini Kenya.
Prof Maathai pia katika uhai wake alipata tuzo mbalimbali za kimataifa kwa kutambua mchango wake.
Prof. Wangari Muta Maathai alianzisha vuguvugu la Green Belt mnamo mwaka 1977, ambapo alifanya kazi na wanawake kote nchini kuboresha maslahi yao na kuhifadhi mazingira.
Alikuwa mtetezi mashuhuri wa matumizi bora ya mali asili . Shughuli zake zilitambuliwa mara kwa mara kote duniani

Rais Jakaya Kikwete Amaliza Ziara Yenye Mafanikio Makubwa Nchini Marekani Nakurejea Nyumbani

 Rais Kikwete akiagana na wafanyakazi wa hoteli ya Jumeirah Essex House jijini New York alipofikia

 Rais Kikwete akiagana na mmoja wa maafisa wa hoteli hiyo
Rais Kikwete akiagana na Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii wa Zanzibar Mh  Juma Duni Haji ambaye ni mmoja wa viongozi wa juu walioongozana na Rais Marekani
  Rais Kikwete akipeana mikono na msaidizi wake Dr Ndumbaro
Rais akiagana na dada aliyekuwa mhudumu wake katika hoteli hiyo
 Rais Kikwete akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Bernard Membe kabla ya kuondoka
 Rais Kikwete akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Bernard Membe
Rais Jakaya Kikwete akiwa na Mwenyekiti wa Galaxy Corporate Offices Inc Bw Charles H. Gray na  (kushoto) Bw Sonny JW Lee ambaye ni afisa uendeshaji mkuu wa World Fashion Development Programmes, baada ya maongezi leo jijini New York, hawa wakiwa wageni wa mwisho kuonana nao kabla ya kuanza safari ya kurejea nyumbani jana Asubuhi.
Picha Zote na IKULU

Taswira Za Rais Wa Zanzibar Dk Ali Shein Na Mama Salma Kikwete Kwenye Uzinduzi Wa Shule ya Sekondari ya Wama Nakayama katika Kijiji Cha Nyamisati wilayani Rufiji

Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein akiwa amefungua pazia ikiwa ni ishara ya kuzindua Shule ya Sekondari ya Wama Nakayama katika Kijiji cha Nyamisati wilayani Rufiji katika Mkoa wa Pwani. Kushoto ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, ambaye ni mlezi wa shule hiyo.
Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein (katik) akipatiwa maelezo na Mwalimu Mkuu Twaha Twaha(kulia) (kus) mama Kikwete.
 
Mama Salma Kikwete Na Waasisi Wa UWT Kwenye ufunguzi wa shule ya Sekondari WAMANAKAYAMA.
Mwanafunzi akifuta machozi wakati akiiwa katika sherehe za uzinduzi wa shule ya sekondari WAMA NAKAYAMA.
Picha na Mwanakombo Juma-MAELEZO

Saturday, September 24, 2011

Rais Kikwete Azindua Rasmi Mkutano wa DICOTA Jijini Washington DC

Rais Jakaya Kikwete akizindua rasmi mpango mpya wa Bima kwa ajili ya Watanzania waishio ughaibuni uitwao Welfare Scheme for Tanzanians in Diaspora (WESTADI).ambapo mwanachama hulipa ada ya dola za Kimarekani 300 kwa mwaka ambazo endapo mwanachama atafariki dunia mwili wake utasafirishwa na NSSF toka huko aliko hadi nyumbani kwake na pia msindikizaji mmoja atalipiwa tiketi ya Ndege
Rais Jakaya Kikwete akihutubia mamia ya Watanzania waishio Marekani wakati wa kufungua rasmi mkutano wa DICOTA 2011 katika ukumbi wa hoteli ya Marriott Hotel and Resort kitongoji cha  Dulles, Virginia, jijini Washington DC.
Rais Jakaya Kikwete akihutubia mamia ya Watanzania waishio Marekani wakati wa kufungua rasmi mkutano wa DICOTA 2011 katika ukumbi wa hoteli ya Marriott Hotel and Resort kitongoji cha  Dulles, Virginia, jijini Washington DC.
Wabunge wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakimshangilia JK wakati nakifungua mkutano wa DICOTA katika ukumbi wa hoteli ya  Marriott Hotel and Resort kitongojini Dulles,Virginia, jijini Washington DC. Kutoka kushoto ni Mbunge wa Bukombe (CHADEMA), Profesa Kulikoyela Kahigi, Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Mh Leticia Nyerere, Mbunge wa Liwale Mh. Faith Mitambo (CCM)  na Mbunge wa Serengeti Dr  Kebwe Stephen Kebwe (CCM)
Sehemu ya umati wa Watanzania wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete wakati akifungua rasmi Mkutano wa DICOTA 2011 katika ukumbi wa hoteli ya Marriott Hotel and Resort kitongojini Dulles,Virginia, jijini Washington DC
Rais Jakaya Kikwete  akiangalia bidhaa ya mafuta maalumu ya kurutubisha na kutunza nywele yaliyobuniwa na kutengenezwa na Mtanzania anayeishi Marekani Bi Lau Kyari  kabla ya  kufungua rasmi mkutano wa DICOTA 2011 katika ukumbi wa hoteli ya Marriot Hotel and Resort kitongoji cha  Dulles,,Virginia, jijini Washington DC. Mjasiriamali huyu, ambaye ni Mkemia bingwa, anatarajia kupeleka Tanzania bidhaa hiyo kabla ya kuanza kutafuta soko la kimataifa
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mmoja wa washiriki katika mkutano huo huku Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Mh Leticia Nyerere akisubiri kwa hamu zamu yake baada ya kufungua rasmi mkutano huo katika ukumbi wa hoteli ya Marriott Hotel and Resort huko Dulles, Virginia, jijini Washington DC
Rais Jakaya Kikwete akigombewa kupewa mikono na Watanzania waishio Marekani baada ya kufungua rasmi mkutano wa DICOTA 2011 katika ukumbi wa hoteli ya Marriott Hotel and Resort huko Dulles in Virginia, jijini Washington DC.
Picha Zote na IKULU
CLICK

Wednesday, September 21, 2011

Wenger Ataka "Miaka Mingine" 14 Arsenal

Arsene Wenger
Arsene Wenger amesema wala hasumbuliwi na kelele zinazopigwa dhidi yake na anataka kuendelea kuingoza Arsenal kwa kipindi kirefu zaidi.
Wachambuzi wa soka wamekuwa wakihoji nafasi ya Wenger wakati huu Arsenal ikishikilia nafasi ya 17 ya msimamo wa Ligi Kuu ya England wakiwa wameuza wachezaji muhimu msimu huu.
Lakini baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Shrewsbury kuwania Kombe la Carling, Wenger amesema: "Sijali kabisa kutokana na uvumi uliopo dhid yangu kwamba nitatimuliwa.
"Nimekuwa katika klabu hii kwa miaka 14 na nimefanikiwa kuiweka katika kuwania ubingwa wa Ulaya kwa miaka hiyo 14. Natumai nitaendelea kuwepo miaka mingine 14."
Mtendaji mkuu wa Arsenal Ivan Gazidis ameiambia BBC kwamba kumfukuza Wenger sio jambo wamalofikiria kulitekeleza.
Zaidi anachokiangazia zaidi Wenger ni kuimarisha kikosi chake baada ya nahodha wake Cesc Fabregas kuhamia Barcelona na kiungo mwenzake Samir Nasri kujiunga na Manchester City mwezi wa Aprili.
Katika siku ya mwisho ya usajili, kiungo wa Everton Mikel Arteta, mshambuliaji Park Chu Young, beki wa kushoto Andre Santos na mlinzi wa kati Per Mertesacker walijiunga na Arsenal, wakati Wenger pia alimchukua kwa mkopo Yossi Benayoun kutoka klabu ya Chelsea.
Lakini mabadiliko hayo yamekuwa makubwa kuyazoea uwanjani, wakati Arsenal imeshinda mechi moja tu ya Ligi kati ya mechi tano huku ikiwa imefungwa mabao mengi hadi sasa.
Wenger amesema:"Naelewa watu hawana furaha na wanalaumu, lakini najua mnafahamu kama ninavyofahamu kwamba watu wanakuwa wepesi sana kufikia hatua ya kulaumu".
"Tunapofanya vizuri tunashangiliwa na kupongezwa, kwa hiyo tunawajibika kukubali lawama iwapo mambo yanapokwenda kombo - lakini kwa pande zote mbili pia tunatakiwa kuwa na subira.

Sunday, September 18, 2011

Taswira Kutoka Viwanja Vya Ikulu Jijini Dar es Salaam Muda Mfupi Baada Ya Kuapishwa Kwa Wakuu Wapya Wa Mikoa na Rais Jakaya Kikwete


Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal akiteta na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika sherehe za kuwaapisha wakuu wa mikoa zilizofanyika ikulu jijini Dar es slaam Septemba 16,2011.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa wa zamani, Daniel Ole Njoolay (kushoto) akiteta na Mkuu wa mkoa huo wa sasa, Stella Manyanya katika sherehe za kuwaapisha wakuu wa mikoa zilizofanyika Ikulu jijini Dar es salaam Septemba 16,2011.
Rais JakayaKikwete akiteta na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika sherehe za kuwaapisha wakuu wa mikoa zilizofanyika ikulu Jijini Dar es salaam Septemba 16,2011.
Picha na Ofisi Ya Waziri Mkuu

WAKUU WAPYA WA MIKOA WAAPISHWA


Rais Jakaya Kikwete, (kulia) akiweka saini kiapo cha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza mara baada ya kumuapisha Ikulu, Dar es Salaam.Wa pili kulia, Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo akishuhudia.Picha na Yusuf Badi

Wednesday, September 14, 2011

Train Collision in Southern India Kills 10

A passenger train collided with another train stopped at a signal in southern India, killing 10 people and injuring dozens.

Rescue workers and others crowd next to the derailed compartments of a passenger train after two trains collided near Arakkonam, southwest of Chennai, India, Wednesday, Sept. 14, 2011. The passenger train traveling through southern India collided with another train stopped at a signal on Tuesday, killing eight people and injuring dozens more, a government official said. (AP Photo/Aijaz Rahi)

BENKI YA NMB YATOA MSAADA WA MILIONI 20 MAAFA ZANZIBAR

Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Alli Iddi akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shillingi Millioni 20, kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Jamii-NMB Shy-Rose Bhanji ikiwa ni msaada wa benki hiyo kwa wahanga kufuatia ajali ya meli huko Zanzibar. Kushoto ni Meneja wa NMB tawi la Zanzibar.Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Alli Iddi akiangalia mfano wa hundi yenye thamani ya Shillingi Millioni 20, aliyokabidhiwa kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Jamii-NMB Shy-Rose Bhanji ikiwa ni msaada wa benki hiyo kwa wahanga kufuatia ajali ya meli huko Zanzibar. Kushoto ni Meneja wa NMB tawi la Zanzibar
Maafisa wa NMB wakiteta jambo na Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi baada ya makabidhiano
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano benki ya NMB,Shy-Rose Bhanji akitia saini kitabu cha maombolezo

Tuesday, September 13, 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA JENGO LA MIHADHARA LA DUCE MILLIONI 158 ZACHANGWA KUSAIDIA UJENZI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua Jengo la Mihadhara na kuchangisha fedha za ujenzi wa Maabara ya Shule ya Sekondari Chang’ombe, wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika katika Chuo Kikuu Kishiriki cha DUCE jijini Dar es Salaam leo Septemba 13, 2011. Kusho ni mwakilishi wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha UDSM, Prof. Yunus Mgaya na (kulia) ni Mkuu wa Chuo hicho Kikuu Kishiriki cha DUCE, Prof. Salome Misana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuzindua Jiwe la Msingi la Jengo la Mihadhara la Chuo Kikuu Kishiriki cha DUCE, uzinduzi uliambatana na uchangishaji fedha kwa ajili ya ujenzi wa Maabala ya Shule ya Sekondari Chang’ombe, ambapo katika zoezi hilo la uchangishaji fedha Makamu alichangia Sh. Milioni 10, na kufanya jumla ya michango kufikia Sh. Milioni 158.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea mchango wa sh. 60,000 uliotplewa na watoto wa Shule ya awali ya Duce kutoka kwa mtoto, Edna Mayungi, wakati wa zoezi la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Maabala ya Shule ya sekondari Chang’ombe lililofanyika wakati wa uzindu wa Jengo la Mihadhara la Chuo Kikuu Kishiriki cha DUCE leo Septemba 13 jijini Dar es Salaam. Katika zoezi hilo zilipatikana jumla ya Sh. Milioni 158 kwa njia ya ‘Cash’ Ahadi na Mnada. Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Terezya Huvisa (kushoto) Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadick.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha DUCE, Prof. Salome Misana, baada ya kuzindua rasmi Jengo la Mihadhara la chuo hicho na kuendesha zoezi la uchangishaji fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Maabala ya Shule ya Sekondari Chang’ombe jijini Dar es Salaam leo Septemba 13.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia picha yake iliyoandaliwa maalu kwa ajili ya kupigwa mnada katika zoezi la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Maabala ya Shule ya Sekondari ya Chang’ombe, uliyofanyika sambamba na uzinduzi wa Jengo la Mihadhara la Chuo Kikuu Kishiriki ch DUCE leo Septemba 13. Katika zoezi hilo zilipatikana Jumla ya Sh. Milioni 158 kwa njia ya Mnada, keshi na ahadi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikagua moja ya chumba cha mihadhara kilichopo katika jengo la Mihadhara la Chuo Kikuu Kishiriki cha DUCE, baada ya uzinduzi uliofanyika Chuoni hapo jijini Dar es Salaam leo Septemba 13.
 Watoto wa Shule ya awali ya DUCE, wakiimba ngonjela mbele ya mgeni rasmi, wakati wa uzinduzi huo leo.
Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu Wa Rais

Emirates Organised Static tour For Airbus A340 Plane in Dar es Salaam


Emirates Area Manager, Abdul Aziz Alhaj (C) is being interviewed by media when the airflght company organised  static tour for Airbus A340 plane in Dar es Salaam on Tuesday.
Emirates Area Manager, Abdul Aziz Alhaj (R) addressing the members of press when the airflght company organised  static tour for Airbus A340 plane in Dar es Salaam on Tuesday. Looking on is Emirates Airport manager, Juma Abubakar.

Msaada wa pesa kwa Mtoto Sesilia Edward - Kupata Upasuaji India


 Hoyce Temu akitoa Msaada kwa mtoto Sesilia Edward

 Ndugu Watanzania,

Jumapili tarehe 11 Septemba, kipindi cha Mimi na Tanzania kinachorushwa na Chanel Ten, kilifanya Mahojiano na Mtoto Sesilia Edward mwenye matatizo ya moyo na anahitaji upasuaji wa haraka kuokoa maisha yake. Upasuaji huo unatakiwa kufanyika nchini India.

Jumla ya dola 15 sawa na shilingi milioni 24 za kitanzania zinahitajika kuokoa maisha yake. Kama asipofanyiwa upasuaji wa haraka la sivyo  atapoteza maisha ndani ya Mwezi Mmoja.

Watanzania wameanza kuchanga kumsaidia motto huyu apate matibabu. Kupitia katika simu za mlezi wake anaeishi naye huko Mbagala Bwana Nyarugembe Peter Kambaliko  katika nambari zifuatazo:

Tigo Pesa:-  0715 095797
MPESA:  –  0762 962467
NMB Account: 2072517079
*Hadi sasa zaidi ya shilingi milioni mbili zimekwisha changwa na bado Watanzania wanaendelea.

Chonde chonde Watanzania, hata mia tano ni mchango.
Usiache kutizama marudio ya kipindi Jumamosi saa 12:30 jioni, Chanel Ten ambapo mtasomewa kiasi cha fedha zilizokusanywa. Account ya NMB imefunguliwa kwa ajili ya hitaji hilo na namba za simu pia.