SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, September 9, 2014

KIVUKO KIPYA 'MV DAR ES SALAAM' CHA DAR-BAGAMOYO CHAKAMILIKA, KUWASILI NCHINI BAADA MWEZI MMOJA

Kivuko cha MV.Dar es Salaam kikiwa kimeshushwa majini leo tayari kwa kuanza safari ya kuja nchini Tanzania kutokea nchini Denmark.
ILE ahadi ya Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli ya kununua Kivuko kipya kwa ajili ya kutoa huduma ya usafiri kati ya Jiji la Dar es Salaam na mwambao wa Bahari ya Hindi hadi Bagamoyo imetimia baada ya kukamilika kwa Kivuko cha Mv Dar es Salaam. 
 
Imeelezwa kuwa kivuko hicho cha 'Mv Dar es Salaam' kilichokuwa kikieundwa huko nchini Denmark, kimekamilika na leo kimegusa rasmi majini  na tayari kinatarajia kuanza safari ya kuja jijini Dar es Salaam ambapo kinatarajiwa kuwasili katika ardhi ya Tanzania jijini Dar es Salaam baada ya wiki tatu mpaka nne zijazo kuanzia leo. 

 Aidha imeelezwa kuwa kiivuko hicho kitakuwa ni cha kwanza kwa kuwa na kasi kubwa kuliko kivuko chochote Afrika ya Mashariki na hasa katika Mwambao wa bahari ya Hindi ukiondoa Afrika ya Kusini. 
 
 Kivuko hiki ni muendelezo wa juhudi za Wizara ya Ujenzi za kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kujenga barabara za New Bagamoyo (Kawawa JCT - Tegeta); ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo kasi (Bus Rapid Transit Infrastructure - BRT).
Pamoja na kuanza kwa ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo kasi awamu ya pili ; ujenzi wa ‘Flyover’ ya TAZARA na UBUNGO ; barabara za pete (DSM Outer Ring Roads); barabara ya Dar es Salaam – Chalinze Express way; kupanua barabara ya lami sehemu ya Gerezani (KAMATA – Bendera Tatu) kutoka njia mbili za sasa hadi njia nne; kujenga daraja la Kigamboni linalounganisha Kurasini na Kigamboni, ambalo linatarajiwa kukamilika mwezi wa sita mwakani. 
 Kivuko cha MV.Dar es Salaam kikiwa kimeshushwa majini leo tayari kwa kuanza safari ya kuja nchini Tanzania kutokea nchini Denmark.

0 comments:

Post a Comment