SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, September 19, 2014

Akon kusambaza umeme Kibera Kenya

10394047_915466105148610_4585435289872044774_n
Rais Uhuru Kenyatta akiwa kwenye mazungumzo na msanii Akon kwenye Ikulu yake jijini Nairobi.(Picha zote kwa hisani ya ukurasa wa Facebook wa Rais Uhuru Kenyatta).

Na Mwandishi wetu
Mwanamuziki nyota wa R&B kutoka Marekani mwenye asili ya Senegal, Akon amekutana na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na kufanya mazungumzo nae juu ya mpango kusambaza umeme katika eneo la Kibera na sehemu nyingine za vijijini zisizokuwa na nishati hiyo.
Mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wake wenye lengo la kugawa umeme kwa mamilioni ya kaya katika bara la Afrika mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka.
”Napenda kumpongeza Akon kwa kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wa kiafrika na napenda kuwatia moyo wengine kuiga mfano wake. Sisi tunaukaribisha mpango huu na tutakuwa nae bega kwa bega” aliandika Rais Uhuru kwenye ukurasa wake wa Facebook.
10472957_915466138481940_7398338281766763319_n
10371359_915466221815265_4675424780169801868_n
Rais Uhuru Kenyatta kwenye picha ya pamoja na Akon.
10406677_915466255148595_2650786118532577845_n
Rais Uhuru Kenyatta akimtembeza Akon kwenye baadhi ya maeneo ya Ikulu ya nchini Kenya mara baada ya mazungumzo.

CHANZO: HIKI HAPA

0 comments:

Post a Comment