SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, May 16, 2010

TUZO ZA KILIMANJARO MUSIC AWARD

Shoo ilikuwa bab-kubwa katika swala zima la burudani kama unavyoona.
Lamar alipata tuzo ya mtayarisha bora wa muziki kwa mwaka 2008, na tuzo hiyo alikabidhiwa na Wakuvanga kutoka Komedy Show.
Meza ambayo alikuwa amekaa Sean Kingstone ilikuwa hii, alikuwa amekaa na wanyamezi wake.

Sean Kingstone akiongea na watanzania na akiwatambulisha watu waliokuja nao kabla ya kuitoa tuzo ya wimbo bora wa ragga DJ wa Sean Kingstone akimtaja mshindi wa ragga ambaye alikuwa ni Bw. Misosi na wimbo wake wa Mungu yuko Bize.
Sean Kingstone akimkabidha zawadi Bw. Misosi. Joh Makini alichukua tuzo ya wimbo bora wa Hip Hop
Chidi Benz alichukuwa tunzo ya msanii bora wa Hip Hop na alikabidhiwa na Sebbo
Hasheem Thabeet yeye alitoa tuzo kwa Video bora kwa mwaka 2008 ambayo ilikwenda kwa CP na wimbo wake wa Problem hapa CP akizungumza machache baada ya kuchukua tuzo.
Diamond akachukua tuzo ya wimbo bora wa mwaka, jamaa alichukua tuzo 3.
AY akiongea mambo fulani kwa wageni rasmi akiwa amesindikizwa na Mwana FA na Prof Jay. 
Na Dj Choka.

0 comments:

Post a Comment