SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, May 16, 2010

MAHAFALI YA WAHITIMU WA JUMUIYA YA TSAH 2010 YATAFANYIKA HAPA!!

Hatimaye Mwenyekiti wa kamati ya muda ya mahafali kwa mwaka huu Mh.Mustafa Said(Matata)ametangaza rasmi sehemu itayofanyika mahafali kwa wahitimu wa mwaka huu tarehe 26/6/2010 kama inavyoonekana pichani,sehemu hii inaitwa LEONIA RESORT.
Jamanii panavutia kwa kweli kamati imeahidi makubwa ndani yake mnaombwa wanajumuiya wote kujitokeza kwa wingi, kila mwanajumuiya anatakiwa kuchangia kiasi cha 800 Rupees.
Wanaopenda kucheza kifupi kuogelea swimming  kazi kwenu.
Sehemu kubwa sana makadirio kwa wanochezea maji wanasema humu wanaweza kuingia watu zaidi ya 160.
Sehemu ya mapumziko imetulia pia,kwa mbele yake kwa wale wanaopenda kujirusha na maji mtafurahi siku hiyo..
Mandhari tulivu  ndani ya Leonia Resort  kama yanavyoonekana.
Sehemu ya chakula hiyo mwanajumuiya usingoje kuadithiwa njoo ujionee mwenyewe.
Baadhi ya viwanja vya michezo,viwanja vyote vya michezo vipo ndani ya Leonia Resort.
Hawa ni baadhi ya wanakamati waliokwenda kukagua,mbele kabisa Bw.Daniel Masimbusi,anaefuata Bi.Neema,nyuma mbele Bw.Dunstan na anaefuata Bi.Joharia Nkya.
Wakiwa ndani kwa ukaguzi zaidi.
Bi.Neema na Bi.Joharia wakipata kumbukumbu ya pamoja baada ya kumaliza ukaguzi huo.
Imetayarishwa na kamati TSAH 2010.

0 comments:

Post a Comment