SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, June 29, 2010

  Waziri Mkuu wa Kenya alazwa hospitalini

Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga
Hadi sasa Raila Odinga mwenye umri wa miaka 65 amekuwa ni mtu mwenye nguvu.
Katika miezi ya hivi karibuni amekuwa akipigia debe katiba mpya inayopendekezwa na hajaripotiwa kuwa na matatizo ya kimwili.
Kwa hiyo taarifa iliyotolewa hii leo na msemaji wake imewashangaza wengi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo madaktari wameamuru Odinga alazwe hospitalini kwa muda wakisema tu kwamba ana uchovu. Cha kukanganya ni kwamba taarifa hiyo iliwanukuu madaktari hao pia wakisema Odinga ana uwezo wa kufanya kazi kama kawaida ikiwa atajisikia kufanya hivyo. Japo hawatamruhusu kufanya hivyo.
Hadi sasa, maswali mengi kuhusu afya ya kiongozi nchini Kenya yameelekezwa kwa Rais Mwai kibaki ambaye baada ya uchaguzi wa mwaka 2003 kulikuwa na tetesi kwamba alipata kiarusi.
Hata hivyo maafisa wake walikanusha madai hayo wakisema alikuwa na matatizo madogo tu ya kiafya.
******************************
Luanda, Angola mji ghali zaidi duniani
Jiji kuu la Angola Luanda


 Utafiti wa kimataifa umebaini kuwa Luanda,mji mkuu wa Aangola ndiyo mji wenye gharama ya juu kwa wataalamu wanaotoka nje na kwenda kufanya kazi huko.
Ripoti iliyonadiwa na kampuni ya masuala ya kifedha ya - Mecer imesema gharama za kupanga nyumba mjini Luanda ni mara dufu ikilinganishwa na jiji la London.
Mji wa Luanda umetajwa kuwa ghali zaidi, ukifuatwa na Tokyo, Ndjamena na Moscow. Bara Afrika lina miji mitatu miongoni mwa miji kumi ambayo ni ghali duniani.
Jiji la Libreville, Gabon likishikilia nafasi ya saba. Uchunguzi ulifanyiwa katika miji 214 katika mabaraza yote matano. Mambo yaliyoangaziwa ni pamoja na gharama za maisha ikiwemo usafiri, chakula, mavazi na starehe.
Tiketi moja ya kutazama filamu mjini Luanda inauzwa dola 13.
Licha ya raia wengi wa Angola na Gabon kuishi katika lindi la umasikini, hali ni tofauti kwa wageni ambapo gharama za maisha miongoni mwa wafanyakazi wa kampuni za mafuta zinaambatana na usalama wao pamoja na ada ya kuagiza bidhaa kutoka nchi zao.
Gharama za juu zimawalazimu wenyeji wengi kuondoka mijini kwani hawawezi kukimu maisha.

0 comments:

Post a Comment