SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, December 1, 2016

MALIGHAFI YA MISITU HAKUNA KUSAFIRISHWA NJE YA NCHI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe wa pili kulia akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa kwanza kulia)  wakiwa kwenye mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam wa kutathmini mafanikio na changamoto  zinazoikabili sekta ya maliasili nchini  tangu novemba 2015 hadi novemba 2016, uliowakutanisha wadau wa Maliasili kutoka sekta binafsi na Serikalini kujadili  sekta za misitu , wanyampori pamoja na  mambo kale ( Picha na Lusungu Helela- Maliasili)
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Eng. Angelina Madete  akichangia hoja kwenye mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam wa kutathmini mafanikio na changamoto  zinazoikabili sekta ya maliasili nchini  tangu novemba 2015 hadi novemba 2016.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe wa akiwa na wadau wa Maliasili wakisiliza kwa makini  uwasilishaji wa mada kuhusu  sekta za misitu , wanyampori pamoja na  mambo kale  kwenye mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam wa kutathmini mafanikio na changamoto  zinazoikabili sekta ya maliasili nchini  tangu novemba 2015 hadi novemba 2016.
Baadhi ya wadau wa Maliasili kutoka serikalini na Sekta binafsi wakifuatilia kwa makini uwasilishaji wa mada za Maliasili  kwenye mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam wa kutathmini mafanikio na changamoto  zinazoikabili sekta ya maliasili nchini  tangu novemba 2015 hadi novemba 2016.



Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amesema Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa hakuna magogo na malighafi ya misitu  yatakayosafirishwa kwenda nje ya nchi kabla ya kuchakatwa.
Amesema , hiyo itasaidia  kuongeza thamani  pamoja na  kupunguza tatizo la  ajira  kwa vijana wengi kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwa ajili ya kutengezea vifaa mbalilmbali vitakanavyo na mazao ya misitu kutokana na Magogo na Malighafi ya misitu kuchakatwa ndani ya nchi.
Amesema hayo leo kwenye mkutano wa kutathmini mafanikio na changamoto  zinazoikabili sekta ya maliasili nchini  tangu novemba 2015 hadi novemba 2016, uliowakutanisha wadau wa Maliasili kutoka sekta binafsi na Serikalini kujadili  sekta za misitu , wanyampori pamoja na  mambo kale
Amesema kuwa  Misitu ni sekta inayokabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ukataji miti hovyo uvunaji haramu wa magogo pamoja na usafirishaji haramu wa magogo kwenda nje ya nchi.
Amesema katika kukabiliana na changamoto hizo Serikali imeanza kuona namna ya  kuwalipa  sekta binafsi na watu  wenye kipato cha chini cha kati watakaokuwa wanapanda miti kama motisha  kutokana na  mchango mkubwa  wa  misitu wa kuzalisha hewa safi duniani kwa  kuondoa hewa ya  ukaa.
Amesema mpango huo kamambe wa kuwalipa watakaopanda miti kwa wingi  itakuwa ni  njia muafaka ya kuondokana na tatizo la ukame linaaloendelea kutokea kutokana miti mingi kuendelea kukatwa kwa ajili ya mkaa na matumizi mengine kuongezeka kwa kasi.

0 comments:

Post a Comment