SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, June 29, 2010

  Milipuko Burundi wakati wa kuhesabiwa kura za urais
Agathon Rwasa, kiongozi wa FNL
Hali ya wasiwasi imetanda mjini Bujumbura,Burundi baada ya mabomu ya guruneti kulipuka katika eneo moja lenye watu wengi jana usiku.
Hakuna aliyekufa kwenye tukio hilo lililotokea wakati shughuli ya kuhesabu kura za urais inaendelea katika sehemu zengine nchini humo.
Kumekuwa na matukio ya mashambulio ya maguruneti katika siku za hivi karibuni.
Wakati huo huo vyama vya upinzani nchini Burundi vimesema kwamba havitatambua matokeo ya urais katika uchaguzi mkuu wa jana ambapo rais Pierre Nkurunziza alikuwa mgombea wa pekee.
Wapinzani wa rais Nkurunziza walijiondoa mchuano wa urais wakidai udanganyifu kwenye uchaguzi wa mabaraza.
Muungano wa vyama 12 vya upinzani umesema ni asili mia 30 pekee ya wapiga kura waliojitokeza kwenye zoezi la jana na kuapongeza raia waliosusia uchaguzi huo.
Uchaguzi wa jana ndiyo wa kwanza tangu kundi la mwisho la waasi kujiunga na mpango wa amani na kuitikia kushiriki katika mchakato wa kisiasa.       
                    ******************

Watu 10 Wakamatwa Marekani kwa kuipelelezea Urusi
Washukiwa kadhaa wamefikishwa mahakamani
Watu kumi wamekamatwa nchini Marekani kwa kushukiwa kuwa majasusi wa Urusi.Watu hao walikamatwa kwenye msako uliofanyika katika miji ya NewYork, Boston, New Jersey na Virginia. Mshukiwa mwingine angali anasakwa.
Idara ya Sheria ya Marekani imetoa stakabadhi kudhibitisha kuwa watu iliowazuilia wamekuwa wakikusanya habari za kijasusi a kuzipokeza kwa serikali ya Urusi.
Idara hiyo inasema baada ya uchunguzi wa muda mrefu imewanasa watu hao wakiwemo wanaume wanne na wake zao ambao wamekuwa wakifanya kazi kichichini ili kupata habari muhimu kutoka kwa ofisi za serikali na idara zingine muhimu.
Maafisa hao wa marekani pia wanasema washukiwa hao wamekuwa wakiwasajili watu wengine kwa kazi hiyo ya kijasusi. Mmoja wao anadai kuwa alikuwa ametumwa kuchunguza hasa jinsi serikali ya Rais Obama inavyoiona Urusi kabla ya rais huyo wa Marekani kuzuru urusi.
Habari hizi zimeitia serikali ya Marekani wasiwasi hasa kwa sababu rais Obama amekuwa akijaribu kuoberesha uhusiano wa serikali hiyo na Urusi.
Matukio haya yanarudisha kumbukumbu ya vita baridi kati ya mataifa hayo ambavyo vilidumu kwa zaidi ya miongo mitatu.
Katika miaka ya 60 hadi ile ya 80 karibu ulimwengu mzima ulijipata umenaswa katika vita hivyo baridi na matai. Mataifa hayo mawili yalikuwa yanang'aninia kuwa na ushawishi na hata udhibiti wa karibu mataifa yote duniani.
Na ili kufanikisha kampeni zao serikali ya Marekani na ile ya muungano wa Usovieti ziliwaweka majasusi karibu kote duniani. Na sasa takriban miaka 20 tangu vita hivyo kukoma mbinu hizo hizo bado zinaendelea kutumiwa.

0 comments:

Post a Comment