SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, June 29, 2010

Robo fainali ya kukata na shoka
Brazil imewafunga Chile mabao 3-1
Robo fainali ya kwanza ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini itakutanisha mabingwa mara tano Brazil na Uholanzi siku ya Ijumaa mjini Port Elizabeth, baada ya timu hizo kufuzu kufuatia ushindi wa Jumatatu.
Brazil iliendelea kudhihirisha azma yake ya kulitwaa kombe hilo kwa mara ya sita ilipowafunga Chile mabao 3-0 katika uwanja wa Ellis Park mjini Johannesburg.
Awali katika uwanja wa Moses Mabhida mjini Durban, Arjen Robben na Wesley Sneider walifunga mabao yaliyoiwezesha Uholanzi kuishinda Slovakia 2-1 na hivyo kujiandikishia nafasi miongoni mwa nane bora.
Mabao ya Brazil dhidi ya Chile yalipatikana kupitia mlinzi Juan aliyefunga kwa kichwa katika dakika ya 38, kabla ya Luis Fabiano kuongeza la pili dakika 4 baadaye.
Robinho alifunga bao la tatu na la ushindi kwa Brazil katika dakika ya 59 kufuatia pasi kutoka Ramires.
Wesley Sneijder
Wesley Sneijder
Uholanzi walionekana kuelekea kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Slovakia hadi muda wa ziada, wakati mlinda mlango Maarten Stekelenburg alipomwangusha Martin Jakubo kwenye eneo la hatari, na hivyo Slovakia wakapata penalti iliyofungwa na Robert Vittek.
Uholanzi haijapata kushinda Kombe la Dunia na imeshafikia hatua ya fainali mwaka 74 na 78, na wakati huu wanajitahidi kutimiza hamu ya kutwaa kombe hilo kwa mara ya kwanza.
Robo fainali nyingine siku ya Ijumaa itakuwa kati ya Ghana na Uruguay katika uwanja wa Soccer City mjini Johannesburg, hii ikiwa ni mara ya tatu katika historia ya Kombe la Dunia kwa timu kutoka Afrika kufikia hatua ya nane bora.
Siku ya Jumamosi itafanyika robo fainali ya tatu kati ya Ujerumani na Argentina katika uwanja wa Green Point mjini Cape Town.
Timu zitakazochuana kwenye robo fainali ya mwisho zitafahamika Jumanne, baada ya mechi za mwisho za raundi ya pili, Paraguay ikicheza dhidi ya Japan mjini Pretoria huku Uhispania na Ureno zikipambana mjini Cape Town.
**************************** 
Blatter aomba radhi kwa makosa ya waamuzi
Sepp Blatter
Rais wa Fifa, Sepp Blatter
Rais wa shirikisho la soka duniani Sepp Blatter ameomba msamaha kwa ajili ya makosa yaliyofanywa na waamuzi kwenye Kombe la Dunia, ambapo bao llilofungwa na Frank Lampard wa England dhidi ya Ujerumani lilikataliwa, na pia kukubaliwa kwa bao la kuotea lililofungwa na Carloz Tevez wa Argentina dhidi ya Mexico.
Bwana Blatter amesema mdahalo kuhusu haja ya kutumia teknolojia kubaini iwapo mpira umevuka mstari wa goli au la utaanzishwa upya kwenye mkutano wa bodi ya kimataifa ya vyama vya soka utakaofanyika mwezi Julai.
Mkutano wa bodi hiyo uliofanyika mwezi Machi uliamua kukataa kutumika kwa teknolojia hiyo kwenye Kombe la Dunia, kwa tetesi kwamba kusimamisha mechi kwa ajili kuthibitisha kwenye video ikiwa mpira umevuka mstari au la kutaathiri mtiririko wa mchezo na pia kuzinyima timu fursa ya kufunga.
Mjadala kuhusu haja ya kutumika kwa teknolojia hiyo uliibuka tena siku ya Jumapili wakati Ujerumani ilipoifunga England mabao 4-1 mjini Bloemfontein na kuiondoa kwenye mashindano.
Kwenye mechi hiyo, mwamuzi kutoka Uruguay Jorge Larriando na msaidizi wake walikataa kutambua kwamba mpira uliopigwa na Frank Lampard katika dakika ya 38 ulivuka mstari wa lango la Ujerumani na kuingia kabla ya mlinda mlango kuuondosha.
Bao hilo lingeiwezesha England kusawazisha kabla ya mapumziko.
Baadaye siku hiyo katika uwanja wa Soccer City mjini Johannesburg kulitokea utata mwingine kwenye mechi kati ya Argentina na Mexico.
Mwamuzi aliruhusu bao la kwanza la Argentina lililofungwa na Carlos Tevez akionekana kuwa ameotea.
Kulitokea mabishano makali uwanjani wakati wa mapumziko baada ya tukio hilo kuonyeshwa tena kwenye skrini kubwa ndani ya uwanja.
Blatter amesema amezungumza na vyama vya soka vya England na Mexico na kuomba msamaha.

0 comments:

Post a Comment