Waziri wa Afya Mh. Seif
Rashid akiongea na Wauguzi wa Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke,
Wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm pamoja na wadau mbalimbali
wakati wa uzinduzi rasmi wa Radio hiyo, ambayo lengo lake ni kuwakomboa
vijana wa mtaani pamoja na vipindi vingine vya kuelimisha Jamii na
Burudani, Pia amewashukuru kwa kutoa msaada wa vifaa mbalimbali ambavyo
vitasaidia katika Hospitali hiyo Tarehe 1.11.2014
Mkurugenzi wa Sibuka George
Ndagali akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ghetto Radio ya
Sibuka Fm iliyofanyika katika katika Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke
ambapo Ghetto Radio imeweza kufunguliwa rasmi katika Mkoa huo na kuweza
kutoa msaada vifaa Mbalimbali pamoja na Madawa ambavyo vyote kwa ujumla
vimegharimu kiasi cha Shilingi Milioni sita na Laki sita.
Mkurugenzi wa Ghetto Radio Matt Brouwer akizungumza neno wakati wa uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm ambapo Bw.Brouwer Alisema kuwa Ghetto Radio ilianzishwa nchini Kenya Miaka Sita iliyopita nakuweza kuwasaidia vijana mbalimbali Hivyo wameweza kuingia nchini Tanzania Iiikuendeleza kuwapa vijana Fursa Na elimu inayotolewa na kituo hicho kwa hapa nchini.
Mkurugenzi wa Ghetto Radio Matt Brouwer akizungumza neno wakati wa uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm ambapo Bw.Brouwer Alisema kuwa Ghetto Radio ilianzishwa nchini Kenya Miaka Sita iliyopita nakuweza kuwasaidia vijana mbalimbali Hivyo wameweza kuingia nchini Tanzania Iiikuendeleza kuwapa vijana Fursa Na elimu inayotolewa na kituo hicho kwa hapa nchini.
Mganga
Mkuu wa Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke Amaani K. Malima akitoa neno
la Shukurani kwa Timu nzima ya Ghetto Radio ya Sibuka Fm kwa kufanya
uzinduzi wa Radio yao katika Hospitali hiyo pia kutoa Msaada wa vitu
mbalimbali vitakavyo saidia katika eneo hilo.
Meneja wa Ghetto Radio ya
Sibuka Fm Edward Lukaka akitoa maelezo machache ya malengo ya Radio
hiyo pia kueleza mikakati ya kuendelea kutoa msaada wa vifaa mbalimbali
vya tiba katika Vituo zaidi vya Afya.
Mkurugenzi wa kituo cha
afya cha Iran Nchini Tanzania Dkt. Farhad Arjomandi akiwashukuru Ghetto
Radio ya Sibuka FM kwa kuanzisha Kituo hicho pia na wao wametoa vifaa
vya matibabu kwa ajili ya kushiriki uzinduzi huo wa Radio.
Mwenyekiti wa Red Cross Mkoa wa Dar es salaam Leonard Masonu akitoa neno la Shukurani.
Hivi
ni Baadhi ya vitu ambavyo vimetolewa na Ghetto Radio ya Sibuka Fm
katika Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke wakati wa uzinduzi rasmi wa
Radio hiyo.
Waziri
wa Afya Mh. Seif Rashid akikabidhiwa rasmi msaada wa vifaa na vitu
mbalimbali vitakavyo tumika katika Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke
kutoka kwa Ghetto Radio ya Sibuka Fm.
Waziri wa Afya Mh. Seif Rashid (kushoto) akishukuru kwa vifaa hivyo.
Baadhi ya Wadau mbalimbali walioshiriki katika Sherehe hiyo ya Uzinduzi Rasmi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm.
Baadhi ya Wauguzi wakiwa katika uzinduzi huo rasmi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
Wafanyakazi
wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm pamoja na wadau mbalimbali wakijiandaa
kuelekea kutoa Msaada wa vitu mbalimbali katika vyumba vya wagonjwa.
Wakiwa wanaelekea Wodini.
Kulia
ni Mkurugenzi wa Sibuka George Ndagali akiwa katika Wodi ya watoto
kukabidhi zawadi za watoto na mama zao, katikati ni Mwanamuziki Mkongwe
wa Bongo Flava Juma Nature ambaye ni Balozi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
Balozi
wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm Juma Nature akiwa anatandika Shuka moja
wapo katika Wodi ya watoto kuashiria kukabidhi mashuka hayo.
Baadhi ya Timu ya wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm.
0 comments:
Post a Comment