SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, November 19, 2011

Saif Al-Islam Gaddafi Amepatikana

 Saif al-Islam Gaddafi
Serikali ya muda ya Libya inasema kuwa Saif al-Islam Gaddafi, mtoto wa kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, amekamatwa.

Waziri wa Sheria wa serikali ya mpito, Mohammed al-Allagi, alisema kuwa Saif al-Islam amezuwiliwa karibu na mji wa Ubari, kwenye jangwa la kusini-magharibi mwa nchi.

Ripoti moja ilieleza kuwa hivi sasa amechukuliwa kwa helikopta kupelekwa Zintan, kaskazini mwa nchi.

Amekuwa akijificha tangu wapiganaji wa serikali ya mpito kuuteka mji mkuu, Tripoli, mwezi Agosti, na anasakwa na Mahakama ya Uhaini ya Kimataifa, kwa mashtaka ya uhalifu wa kivita.
Chanzo BBC SWAHILI.

0 comments:

Post a Comment