Mchezaji wa Manchester City Sergio Aguero akishangilia goli katika ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Manchester United
Manchester
City imeendeleza ubabe wake dhidi ya majirani zao Manchester United kwa
kuwachapa goli 1-0 katika mchezo mkali uliofanyika katika uwanja wa
Etihad, Jumapili.
Sergio Aguero aliipatia timu yake goli hilo katika dakika ya 63 ya mchezo.
Goli hilo
la kumi kwa Aguero katika msimu huu wa ligi kuu ya England liliivunja
Manchester United iliyokuwa na ngome iliyosambaratika baada ya Chris
Smalling kutolewa nje kwa kadi nyekundu katika kipindi cha kwanza cha
mchezo na Marcos Rojo kutolewa nje katika machela baada ya mapumziko
kutokana na kuumia bega.
Chris Smalling wa Manchester United akionyeshwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Manchester City, Jumapili
Ushindi
huu wa Manchester City pia unatoa mwanga wa matumaini kwa kocha Manuel
Pellegrini ambaye wiki iliyopita, timu yake ilipoteza kwa West Ham
katika mchezo wa ligi kuu na kisha kutolewa katika kombe la Capital One
baada ya kufungwa nyumbani na Newcastle.
Manchester City walikuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Mchezo
kati ya Manchester City na Manchester United ulikuwa mpambano mkali,
ukiwa wa kwanza kwa meneja mpya wa Manchester United, Louis van Gaal,
akishuhudia ngome ya timu yake ikiyumba na nguvu ya safu ya ushambuliaji
ya kina Angel Di Maria, Robin van Persie na Wayne Rooney ikishindwa
kupeleka michomo iliyotarajiwa katika lango la Manchester City.
Wakati
meneja wa Manchester United akisikitika kwa makosa ya kizembe
yaliyomsababishia Chris Smalling kutolewa nje kwa kadi nyekundu, wenyeji
Manchester City walijawa na furaha kwa kushinda kwa mara ya sita katika
michezo saba iliyozikutanisha timu hizo na pia Manchester City
ikishinda mechi nne mfululizo dhidi ya Manchester United.
Kwa
matokeo hayo Chelsea bado inashikilia usukani wa ligi kuu ya England
ikiwa na pointi 26, pointi sita juu ya Manchester City na pointi nne juu
ya Southampton inayoshikilia nafasi ya pili katika msimamo wa ligi
hiyo.
Manchester
United iko katika nafasi ya kumi baada ya michezo kumi ikiwa na pointi
13, huku Burnely ikiwa katika nafasi ya ishirini na ya mwisho katika
ligi kuu hiyo, kwa kujikusanyia pointi nne tu katika michezo yake kumi
iliyokwishacheza.
Chanzo:BBC
0 comments:
Post a Comment