SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, October 9, 2014

TSN Group yapongeza kuanzishwa kwa mbio fupi katika Rock City Marathon 2014

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh4Pkz4W17zTmVdTrB02AGN8FRqCx-rvL-u7u5dHX4E1vkwn4wErtHfTYVF9IjEDhXJyPPVwUPa221KVMTvEsIfxqVX4kVdG5ul2g134zX_y0NEfzoL9g1rYPGB3HWx8ESBXZG-IkOY9EE/s1600/3.jpg
 Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah (wapili kushoto)akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 13 Mratibu wa Mbio za Rock City Marathon 2014, Bw. Mathew Kasonta (wa kwanza kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Mbio hizo zitafanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Wakishuhudia wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
 Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah  (wapili kulia)akifafanua jambo  kwa waandishi wa habari wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni hiyo kudhamini mbio za Rock City Marathon 2014 zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Wakishuhudia kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, Mratibu wa mbio hizo, Bw. Mathew Kasonta (wapili kushoto) na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
 Mratibu wa mbio za Rock City Marathon, Bw. Mathew Kasonta, (wa pili kushoto) akiongea na waandishi muda mfupi kaba ya kupokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni ya TSN Group kuoitia kinywaji chake cha Chili Willy kama udhamini wa mbio hizo kwa mwaka huu zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah akifuatiwa na Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, na kushoto ni Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
======  =======   =========
Ukurasa mpya umefunguliwa katika mbio za Rock City Marathon za mwaka huu ambapo kwa mara ya kwanza tangu mbio hizo zilipoanzishwa miaka mitano iliyopita, mbio fupi sasa zitakuwepo. 

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 13 kwa waratibu wa mbio hizo kampuni ya Capital Plus International Limited (CPI), Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN Group Bw. Farough Baghozah aliipongeza hatua hiyo, na kusema kuwa kampuni yake inaungana na wadhamini wengine kuunga mkono tukio hilo la kila mwaka sababu ya dhamira yake ya kuibua na kukuza vipaji vya vijana katika riadha na kukuza utalii wa ndani kupitia michezo.

“Tunayofuraha kuidhamini mashindano ya mwaka huu ambayo sasa yatajumuisha na vijana wadogo ambao wana vipaji vya kukimbia mbio fupi fupi. Hii itawapa vijana wengi nafasi ya kuonyesha vipaji vyao, ambavyo vinaweza kuwa ndiyo fani zao hapo mbeleni,” alisema Bw. Baghozah. 

Alisema kuwa kampuni yake imekuwa ikiunga mkono jitihada mbali mbali zinazolenga kukuza sekta ya  michezo na burudani nchini Tanzania, ambayo imekuwa ikitengeneza fursa za ajira miongoni mwa vijana walio wengi nchini.
 
“Hivi karibuni tu, TSN Group iliweza kuwaleta wachezaji wa timu ya Real Madrid ili kucheza na wachezaji wa zamani wa Tanzania wa mpira wa miguu. Hii ililenga katika kuwatia morari wachezaji wetu na vijana kupenda michezo, wakiendelea kuongeza jitihada ili kufanikiwa zaidi katika kile wanachofanya,” alisema.

Naye mratibu wa tukio hilo, Bw. Mathew Kasonta alisema udhamini huo kutoka TSN Group utasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha mbio hizo za Rock City Marathon 2014, ambapo vipaji katika mchezo wa riadha vitagundulika pamoja na kuyafanya mashindano hayo kuwa chanzo kikubwa zaidi ya kutangaza maeneo mbali mbali ya utalii katika kanda ya ziwa.  

 “Baada ya kupata udhamini toka kwa wadhamini wetu, kamati ya maandilizi ilikaa na kukubaliana kuwa mbio za Rock City za mwaka huu zitajumuisha mbio fupi. Hizi zitajumuisha vijana kutoka katika shule za sekondari na wale waliopo shule za msingi madarasa ya juu. Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kuona kuwa mashindano ya marathon nyingi nchini, hayana mbio fupi ambazo zina vipaji vingi pia,” alisema Kasonta.   

Alisema mbio hizo fupi zitakuwa ni; kilomita 100, kilomita 400 na kilomita 1500. Mbio hizo zitafanyika baada ya mbio ndefu ya nusu marathoni. Bw. Kasonta alisema fomu za usajili zinapatikana katika ofisi za kampuni ya Capital Plus International Limited (CPI) jengo la ATC ghorofa ya tatu jijini Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza, Ofisi zote za wilaya za Michezo na Utamaduni mkoani Mwanza, Uwanja wa Nyamagana na pia zinapatikana katika mtandao wa  www.therockcitymarathon.blogspot.com.  

“Meya wa jiji la Mwanza, Bw. Stanslaus Mabula alifungua usajili kwa kuwa mshiriki wa kwanza kujisajili katika mbio za Rock City Marathon 2014 ambazo zitaanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 mwezi Oktoba mwaka huu, ambapo ataonyesha uwezo wake katika riadha kwenye mbio za kilometa 5,” alisema. 

Bw. Kasonta aliwataja wadhamini waliyofanyikisha mbio hizo kuwa ni Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), TSN Group kupitia kinywaji chake cha Chilly Willy, pamoja na African Barrick Gold, IPTL, Air Tanzania, New Mwanza Hotel, Nyanza Bottling, Sahara Media Group, Continental decoders, New Africa Hotel, PPF, Tanapa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).

0 comments:

Post a Comment