SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, November 8, 2011

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Awasili Zanzibar Baada ya Kumaliza Ziara Yake Nchini Marekani

 MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akizungumza na Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, kufuatia kumaliza ziara ya Kiserikali Nchini Marekani jana.
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdalla Mwinyi Khamis, alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea ziarani Marekani.
Mwandishi wa Redio One na ITV, Farouk Karim akiuliza swali wakati wa mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais alipowasili Zanzibar akitokea Marekani katika ziara ya Kiserikali, na kuelezea mafanikio ya ziara yake.
Mwandishi wa Gazeti la Serikali, Zanzibar Leo, Mwantanga Ame akimuuliza swali Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi mafanikio ya ziara yake Nchini Marekani.

0 comments:

Post a Comment