SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, April 16, 2014

MKUTANO WA MRADI WA UKANDA WA KATI WA UCHUKUZI JIJINI DAR JANA

 Mkurugenzi Mkuu wa Jukwaa la Uchumi wa Nchi za Afrika,Elsie Kanza akisoma risala ya kumkaribisha Mgeni rasmi Mhe.Rais Jakaya Kikwete katika ufunguzi wa Mkutano wa siku moja wa Mradi wa Ukanda wa kati wa Uchukuzi leo jijini Dar es laam, Mkutano huo ni maandaliza ya mkutano unaotarajiwa kufanyika Abuja ,Ngeria.
 Rais  wa Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania, Jakaya Kikwete  akiongea na wajumbe wa mkutano wa Mradi wa ukanda wa kati wa Uchukuzi  wakati wa ufunguzi wa Mkutano  huo  leo jijini Dar es Salaam,Mradi huo utahusiha nchi za Afrika Mashariki katika ujenzi wa reli.
 Katibu Mkuu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya kusini mwa Afrika  Dkt.Stergomena Lawrence, akiosoma hotuba wakati wa  ufunguzi wa mkutano wa Mradi wa ukanda wa kati wa Uchukuzi   leo jijini Dar es Salaam,Mradi huo utahusiha nchi za Afrika Mashariki katika ujenzi wa reli.
 Mkurugenzi wa kitivo cha taarifa cha nchi za Afrika Mashariki,Grabiel Negatu akiongea na wajumbe wa mkutano wa Mradi wa ukanda wa kati wa Uchukuzi uliofanyika leo jijini Dar es Salaam
 Wajumbe wa mkutano wa Mradi wa ukanda wa kati wa Uchukuzi , uliofanyika  leo jijini Dar es Salaam, wakifuatilia kwa makini mambo mbalimbali wakati wa mkutano huo, unaohusisha ujenzi  wa reli kwa nchi za Afrika Mashariki.
 Mkurugenzi Mkuu wa Jukwaa la Uchumi wa Nchi za Afrika,Elsie Kanza (wa pili kulia) akimuongoza mgeni rasmi Mhe.Rais Jakaya Kikwete  kuelekea katika eneo la picha ya pamoja,baada ya kufungua Mkutano wa siku moja wa Mradi wa Ukanda wa kati wa Uchukuzi leo jijini Dar es laam.
 Rais  wa Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania, Jakaya Kikwete  akisalimiana na Mkurugenzi wa kitivo cha taarifa cha nchi za Afrika Mashariki,Grabiel Negatu (kulia) wakati wa mkutano wa Mradi wa ukanda wa kati wa Uchukuzi  leo jijini Dar es Salaam.
 Rais  wa Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania, Jakaya Kikwete  akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano wa Mradi wa ukanda wa kati wa Uchukuzi  leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Lorietha Lawrence-Maelezo