SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, November 2, 2015

TAMASHA LA UTALII NA AMANI KUFANYIKA NOVEMBA 22 ARUSHA

 mkurugenzi wa kampuni ya  Arusha Media  ambaye ni mmojawapo wa waandaaji wa tamasha hili Musa Juma katikati akiwa anaongea na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha hilo
 Akizungumzia tamasha hilo na kutaja michezo itakayokuwepo  , Mkurugenzi wa  Alfredo Shahanga  Sports Promotion ,Alfredo Shahanga katika kati
 baadhi ya waandishi wa habari wakifatilia mkutano huo
Mratibu wa Tamasha hilo, Andrea Ngobole   katikati akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari awapo pichani

 Na Woinde Shizza,Arusha
TAMASHA la Utalii na amani, Arusha tourism Festival linatarajiwa kufanyika Novemba 22 katika jiji la Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari  Golden Rose hotel , Mratibu wa Tamasha hilo, Andrea Ngobole alisema, tamasha hilo limeandaliwa na taasisi ya Arusha Media na Alfredo Shahanga Sports  Promotion.

Alisema katika tamasha  hilo, kutakuwa na michezo michezo mbali mbali, ikiwepo soka, mashindano ya riadha ya Tourism Marathon, maonesho ya utalii na kongamano la utalii na amani.
"kauli mbiu ya tamasha hili ni Utalii wa ndani na amani sasa tunatoa wito kwa wadau mbali mbali kujitokeza kushiriki"alisema

Akizungumzia tamasha hilo, Mkurugenzi Alfredo Shahanga alisema, maandalizi yote muhimu yamekamilika.

Hata hivyo, alitoa wito kwa wadhamini zaidi kujitokeza  kudhamini ili kuhakikisha wakazi wa Arusha wanashiriki kuhamasisha utalii wa ndani na kuhubiri amani.
Naye mkurugenzi wa kampuni ya Arusha media ambaye pia ni mmoja wapo wa waandaaji wa tamasha hilo alitaja michezo ambayo itakuwepo ni pamoja na kukimbiza kuku,kuruka kamba,kukimbia na magunia ,riadha ambapo alisema kuwa kutakuwa na mbio za kilometa tano,half marathoni pamoja na full marathoni ambapo alieleza kuwa mbio za full marathoni zenyewe zitafanyika siku  december 13.

0 comments:

Post a Comment