SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, May 28, 2015

MKUTANO WA 6 WA WADAU WA GEPF WAANZA LEO JIJINI TANGA

Mgeni Rasmi katika Mkutano wa sita wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Naibu Waziri wa Fedha, Mh. Adam Malima akitoa hotuba yake katika ufunguzi wa Mkutano huo, ulioanza leo Mei 28, 2015 kwenye hoteli ya Regal Naivera, Jijini Tanga. Kauli mbiu ya Mkutano huo ni "Mafao Bora kwa Maisha yako ya Sasa na ya Baadae".
PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Daud Msangi akizungumza wakati akitoa utambulisho wa wageni mbali mbali waliohudhulia kwenye Mkutano wa sita wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, ulioanza leo Mei 28, 2015 kwenye hoteli ya Regal Naivera, Jijini Tanga. 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Joyce Shaidi akitoa taarifa ya Bodi yake kwa wanachama na wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, wakati wa Mkutano wa sita wa Mwaka wa Mfuko huo, ulioanza leo Mei 28, 2015 kwenye hoteli ya Regal Naivera, Jijini Tanga. 
 Mgeni Rasmi katika Mkutano wa sita wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Naibu Waziri wa Fedha, Mh. Adam Malima (kushoto) akizindua rasmi Mafao Mapya yatowewayo na Mfuko huo, mara baada ya kuufungua Mkutano huo.Wengine pichani toka kulia Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Daud Msangi, Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii, Juma Muhimbi pamoja na  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Joyce Shaidi.
Picha ya pamoja.
 Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Aloyce Ntukamazina akielezea jambo juu ya muonekano wa logo mpya ya Mfuko huo, iliyozinduliwa rasmi leo Mei 28, 2015 kwenye hoteli ya Regal Naivera, Jijini Tanga. 
 Muwakilishi wa Wakuu wa Mifuko ya Hifadhiza Jamii nchini, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa PPF, William Erio akitoa shukrani kwa Mgeni Rasmi pamoja na wadau wote waliohudhulia kwenye Mkutano huo.
Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dkt. Fatma Mrisho pia alipata wasaa wa kutoa salamu zake kwa wadau wote waliohudhulia kwenye Mkutano huo.
Mgeni Rasmi katika Mkutano wa sita wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Naibu Waziri wa Fedha, Mh. Adam Malima (wa pili kushoto) akikabidhi tuzo kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, SACP Zuber Mwombeji kwa niaba ya Jeshi la Polisi lililoongoza kuwa wachangiaji bora wa Mfuko huo.
Mgeni Rasmi katika Mkutano wa sita wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Naibu Waziri wa Fedha, Mh. Adam Malima akimkabidhi tuzo Mwanachama wa GEPF anaechangia kwa hiari, Chipegwa Chitojo.
Mgeni Rasmi katika Mkutano wa sita wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Naibu Waziri wa Fedha, Mh. Adam Malima akimkabidhi tuzo wakala wa Mfuko wa GEPF, Said Omar Mwagajiko.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, Daud Msangi akiteta jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii, Juma Muhimbi wakati wa Mkutano wa sita wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF, ulioanza leo Mei 28, 2015 kwenye hoteli ya Regal Naivera, Jijini Tanga.

Baadhi ya Wakuu wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii wakiwa kwenye Mkutano huo.

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Mh. Joshua Nassary akifatilia kwa makini Mkutano huo.

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa GEPF, Anselim Peter akifatilia ufunguzi wa Mkutano huo.
Sehemu ya Wadau na Wanachama wa Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF wakiwa kwenye Mkutano huo, ulioanza leo Mei 28, 2015 kwenye hoteli ya Regal Naivera, Jijini Tanga. 
Burudani ya ngoma.
Picha ya pamoja na Viongozi mbali mbali.
Picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya GEPF.
Picha ya pamoja na Washindi wa Tuzo za Uchangiaji bora.
Wadau na Wanachama wa Mfuko wa GEPF.
Picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Mfuko wa GEPF.
Na michuzi matukio

0 comments:

Post a Comment