SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, October 17, 2014

SNV yazindua ushirikiano na FINCA kuanziasha mradi wa kuboresha maisha ya vijana 20500 waishio vijijini

1
Mkuu wa Huduma za Kibenki wa FINCA Tanzania, Bwana Gershom Mpangalah akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mradi wa kusaidia vijana wa OYE unaofanywa kati ya FINCA na shirika la maendeleo la SNV. Wanaotazama kutoka kushoto ni Mkuu wa Mradi OYE Upande wa Vijana Bwana Awadh Milas, Mkuu wa Miradi ya OYE Tanzania, Mozambique na Rwanda, Bwana Roy Van Der Drift na Mkurugenzi Mtendaji wa FINCA Bwana Ed Greenwood.

Na Mwandishi wetu
Shirika la Maendeleo la Kiholanzi SNV na Mshirika wake Master Card Foundation limezindua ushirikiano na FINCA M.F.C. Tanzania wenye lengo la kusaidia vijana walioko nje ya mfumo wa shule katika mradi unaoitwa Fursa za Ajira kwa Vijana (OYE) ambao utasaidia ajira kwa vijana zaidi ya 20,500 wanaoishi vijijini
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Meneja wa Mradi wa OYE Tanzania, Msumbiji na Rwanda, Bwana Roy Van Der Drift, alisema ushirikiano baina ya SNV na FINCA Tanzania ni kwa ajili ya kutekeleza mradi wa OYE kwa miaka mitano katika nchi za Tanzania, Msumbiji, Na Rwanda na utajikita katika kuwapa vijana ujuzi kuhusu soko la fursa za ajira na kuwasaidia kuanzisha biashara mpya.
‘Mahusiano yetu na FINCA Tanzania yanalenga kutekeleza mradi wa OYE, na lengo kuu ni kuhamasisha, kutia nguvu na kuhimiza vijana wa vijijini kubuni na kubadilisha masoko yaliyopo na kutengeneza mapya” alisema Drift.
Ushirikiano wa SNV na FINCA Tanzania, unalenga kuwawezesha vijana kufikia huduma za kifedha, ushauri wa kibiashara na mafunzo yenye kuwajengea uwezo na kujiamini na kuchangamkia fursa za masoko ya kilimo na nishati mbadala.
3
 Mkuu wa Miradi ya OYE Tanzania, Mozambique na Rwanda, Bwana Roy Van Der Drift akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani).
“Biashara ndogondogo zikiendelezwa zinaweza kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana. Mradi huu utatengeneza ajira ambazo zitapunguza umasikini na kuinua kipato miongoni mwa vijana waishio vijinini. Alisema Awadhi Milasi, Mkuu wa Mradi OYE Tanzania upande wa vijana.
Mradi wa OYE ambao uko katika mwaka wake wa pili kiutekelezaji umewapatia mafunzo vijana Zaidi ya 1300 katika Nyanja za teknolojia, biashara ya kilimo na nishati mbadala na unalenga kuwafikia vijana wengi Zaidi katika elimu ya stadi za maendeleo ya biashara ambapo vijana wanaofikia 900 watapata mafunzo mwaka huu.
“Shirika la kifedha la FINCA limekuwa mstari wa mbele kutoa misaada ya kifedha kwa wajasiriamali wadogo kabisa na mpaka sasa linafanya kazi kwenye mikoa 17 na matawi 26. Tuna uhakika kupitia Mradi wa OYE tutawafikia vijana wengi zaidi na kutimiza ndoto zao za kibiashara” alisema Ed Greenwood, Mkurugenzi Mtendaji wa FINCA.
5
SNV ni Shirika la Kimataifa la maendeleo linalofanya kazi katika nchi 35 kwa Africa, Asia na Amerika ya kusini. SNV inajenga uwezo wa serikali za mitaa, vyama vya kiraia na mashirika binafsi katika kuendeleza masoko ambayo yanajumuisha watu wasiojiweza katika kilimo, nishati mbadala na maji safi.

0 comments:

Post a Comment