SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, July 27, 2014

DIAMOND ASHINDA TUZO ZA AFRIMMA ZILIZOFANYIKA MAREKANI

Screen Shot 2014-07-27 at 9.43.50 AMZinaitwa African Muzik Magazine Awards ambapo za mwaka huu 2014 zimetolewa huko Eisemann center Texas Marekani na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali akiwemo Diamond wa Tanzania ambae pia alikua mmoja wa wanaowania tuzo.

Good news za ushindi wote huu ni kwa mujibu wa meneja Babu Tale ambae nae kahudhuria tuzo hizi Marekani alienitumia msg kwa kusema wametangaza ukumbini kwamba Diamond ameshinda tuzo mbili moja ya Msanii bora wa Afrika Mashariki na nyingine ni wimbo bora wa kushirikiana ambao ni ‘number one rmx’ alioufanya na Davido wa Nigeria.
Kolabo bora ni tuzo iliyokua inawaniwa na single ya T Pain na 2 Face – rainbow, Khona ya Uhuru na Mafikizolo wa South Africa, Surulere remix ya Dr Sid wa Nigeria, Mkenya Amani ft. Waganda Radio na Weasel ‘kiboko changu’ J Martins ft. Dj Arafat ‘touching body’ na Rebees na Wizkid ‘slow down’
Tuzo ya msanii bora wa kiume Afrika Mashariki aliyoishinda Diamond ilikua inawaniwa pia na Ben Pol kutoka Tanzania, Bebe Cool wa Uganda, Wyre wa Kenya, Navio wa Uganda na Jackie Gosee wa Ethiopia.
Screen Shot 2014-07-27 at 8.17.01 AMLady Jaydee ameshinda tuzo ya Msanii bora wa kike Afrika Mashariki aliyokua anashindania na Rema wa Uganda, Aster Aweke wa Ethiopia, Avril wa Kenya, Victoria Kimani wa Kenya na Irene Ntale wa Uganda.
Producer bora wa mwaka ni Mtanzania Sheddy Clever aliekua anashindana Dj Oskido wa South Africa, Don Jazzy wa Nigeria, Shizz wa Nigeria, Killbeatz wa Ghana, Oskido wa South Africa, Nash Wonder wa Uganda na Ogopa wa Kenya.
Tuzo ya Mtayarishaji bora wa video imekwenda kwa Ogopa Dj’s ambao ndio waliifanya ile video ya kwanza ya ‘My number 1′ ya Diamond Platnumz.

Stori zaidi na pichaz vitafata baadae hivyo endelea kukaa karibu na millardayo.com mtu wangu ili ujue kilichotokea kwenye tukio hili ambalo limewahusisha wakali wengine kama Davido, 2Face, Fally Ipupa, Iyanya, Flavour, Wyre, Miriam Chemmoss na wengine ambao ni sehemu ya watu kutoka nchi 17 za Afrika
========================
Msanii bora wa kike Afrika Mashariki, Lady Jaydee.
Diamond akiwa na Davido.

STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' ameendelea kufanya vizuri katika tasnia ya muziki ndani na nje ya nchi baada ya kutwaa tuzo ya AFRIMMA 2014 ya Msanii bora wa kiume Afrika Mashariki huku Lady Jaydee akinyakua tuzo ya Msanii bora wa kike Afrika Mashariki.
Diamond wakati akielekea kwenye ukumbi linapofanyika zoezi la utoaji tuzo za Afrimma.

Tuzo hizo za Africa Music Magazine (AFRIMMA) zimetolewa leo alfajiri jijini Richarson, Texas nchini Marekani.

Diamond alikuwa anawania tuzo katika vipengele vitano ambavyo ni: Msanii bora wa mwaka Afrika, Wimbo wa mwaka, Collabo bora, Video bora ya mwaka na Msanii bora wa kiume wa Afrika Mashariki.
Kupitia ukaunti yake ya Instagram, Diamond ameandika hivi:
WASHINDI WA TUZO HIZO ZA AFRIMMA 2014 NI KAMA IFUATAVYO:
Best DJ Africa 2014- Dj Black (Ghana)
Best African DJ USA 2014 – Dj Josh (Kenya)
Best Video of the Year 2014- Flavour (Nigeria)
Best Male East Africa 2014- Diamond (Tanzania)
Best Male West Africa 2014- Davido (Nigeria)
Best Female East Africa 2014- Lady Jaydee (Tanzania)
Best Female West Africa 2014 – Tiwa Savage (Nigeria)
Best Male Central Africa 2014 – Fally Pupa (Congo)
Best Female Central Africa 2014- Gasha ( Cameroon)
Best Male Southern Africa 2014- Khuli Chana (South Africa)
Best African Group 2014- P-square (Nigeria)
Best Male Diaspora 2014- Fuse ODG (Ghana)
Best Female Diaspora 2014- Les Nubians (Cameroon)
Best Female Southern Africa 2014- Zahara (South Africa)
Best Dancehall Artist 2014 – Timaya (Nigeria)
Best Dance in a Video 2014- Iyanya (Lekwa Ukwu) (Nigeria)
Best Gospel Artiste 2014- Bahati (Kenya)
Best Traditional Artist 2014- Flavour (Nigeria)
Best Newcomer 2014- Stanley Enow (Cameroon)
Best Video Director 2014- Ogopa Dj’s (Kenya)
Music Producer of the year 2014- Dj Oskido (South Africa)
Best Dance Group 2014- Imagineto (Nigeria)
Best Rap Act 2014- Sarkodie (Ghana)
Best Collaboration 2014- Mafikizolo ft Uhuru (Khona) (South Africa)
Song of the Year 2014- Kcee (Nigeria)
Artist of the Year 2014- Davido (Nigeria)
Leadership in Music Award 2014- 2face Idibia
Legendary Award 2014- Yvonne Chaka Chaka
Transformational Leadership Award 2014- Chief Dr. Godswill Akpabio

0 comments:

Post a Comment