
Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Rajab Katimba
akizungumza na waandishi wa habari jana, kuhusu mambo mbalimbali ikiwa
ni pamoja na mchakato wa Katiba. Kulia ni Wajumbe, Shaban Ibrahim na
Suleiman Abdallah. Picha na Rafael Lubava
---
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania imeungana na maaskofu
mbalimbali kuwataka wajumbe wa Bunge la Katiba kuheshimu Rasimu ya
Katiba iliyowasilishwa kwa mujibu wa sheria na Tume ya Mabadiliko ya
Katiba.
Pia, taasisi hiyo imemtaka Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kujiuzulu nafasi
zake zote za uongozi kutokana na kauli waliyodai ya kichochezi,
aliyoitoa katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma kuwa ukipitishwa
muundo wa serikali tatu, jeshi litachukua nchi kwa sababu itashindwa
kuwalipa mishahara.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Msemaji
wa Jumuiya na Taasisi hizo, Sheikh Rajab Katimba alilaani kauli kuhusu
jeshi na kuwa makanisa yote yatafungwa na nchi itakosa amani kutokana na
kupitisha muundo huo wa serikali.
Kwa habari zaidi bofya na Endelea.....



