SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, March 30, 2014

Serikali kujenga Bandari ya Mwambani

DSC03048
Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Freddy Liundi (wa pili kutoka kushoto) akitoa maelezo juu ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Bandari ya Mwambani kwa kiongozi wa timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo  kutoka Tume ya Mipango ambaye ni Naibu Katibu Mtendaji anayesimamia Kongane ya Sekta za Uzalishaji, Bw. Maduka Kessy.
DSC03049
Timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo, kutoka Tume ya Mipango wakiongozwa na Naibu Katibu Mtendaji, Bw. Maduka Kessy (wa kwanza kushoto) wakipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa bandari ya mwambani ambapo upembuzi yakinifu tayari umeshafanyika.
DSC03063
Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga akionesha eneo ambapo bandari ya Mwambani itajengwa.
DSC03085
Picha ikionesha eneo la mwambani ambako ndipo miundombinu ya bandari itajengwa.
DSC03087
Timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Tume ya Mipango wakisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Bw. Freddy Liundi (wa pili kulia) ufukweni mwa bahari, eneo ambapo bandari ya Mwambani itajengwa.(Picha na Joyce Mkinga).