SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, January 15, 2014

Abiria 48 wanusurika kufa kwenye ajali ya basi la Shabiby

E83A6439
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi (mbele ya basi lililopinduka aliyenyoosha mkono) akiangalia basi la Shabiby lililopinduka eneo la kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida.Basi hilo ambalo lilijeruhi abiria 28 akiwemo kondakta aliyevunjika miguu yote, lilipinduka katika harakati zake za kulipita basi jingine.

E83A6449
Lori la mafuta lililogongwa na basi la Shabiby na kusababisha abiria 28 kujeruhiwa.
E83A6435
Kondakta wa basi la shabiby Tadei Mhando aliyevunjika miguu yote miwili baada ya basi hilo kupinduka eneo la kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida. Waauguzi wa hospitali ya mkoa mjini hapa,wakimpeleka kondakta Tadei Mhando chumba cha upasuaji.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
ABIRIA 48 wa basi la kampuni ya Shabiby lifanyalo safari zake kati ya mkoa wa Arusha na Dodoma, wamenusurika kufa baada ya basi hilo kupinduka wakati likijaribu kupita basi jingine.
 Basi hilo aina ya Yutong lenye namba za usajili T.930 BUW, limepinduka katika barabara kuu ya Singida-Dodoma eneo la kijiji cha Kisaki Manispaa ya Singida.
 Ajali hiyo imetokea Januari 13 mwaka huu saa saba mchana wakati basi hilo likitokea mkoani Arusha kuelekea mjini Dodoma.
 Kondakta wa basi hilo,Tadei Mhando amesema kati ya abiria hao,28 wakiwemo watoto wawili,wamepata majeraha katika sehemu zao mbalimbali za miili yao.
 “Mimi ndiye niliyeumia zaidi kuliko majeruhi wote wa basi letu.Nimevunjika miguu yote miwili na sasa natarajia kuingizwa ‘theater’ kwa matibabu zaidi.Tunashukuru hakuna mtu aliyepoteza maisha”,amesema Tadei.
 Akifafanua zaidi juu ya ajali hiyo,Tadei amesema walipofika eneo la tukio la Kisaki ambalo lina mwiinuko huku basi lao likiwa kwenye mwendo kasi,dereva wao alijaribu kulipita basi la princess Muna.
Amesema katika jaribio hilo,mabasi yote mawili yakawa kwenye mwendo kasi unaofanana na wakati huo huo,lori la mafuta lililokuwa linapishana na mabasi hayo,liliibana basi la shabiby na kusababisha ligonge lori hilo ubavuni karibu na kichwa.
 “Kutokana na kubanwa huko huku Shabiby likiwa kwenye mwendo kasi,dereva alishindwa kulimudu na hivyo kusababisha lipinduke na kuharibika vibaya”,alifafanua Tadei.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi na kamati yake ya ulinzi, ilifika hospital ya mkoa na kuwapa pole na majeruhi na kisha alienda eneo la tukio Kisaki.

0 comments:

Post a Comment