SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, November 1, 2013

SHUJAA MAREHEMU LUTENI RAJABU AHMED MLIMA AZIKWA MAKABURI YA KISUTU DAR ES SALAAM JANA

    Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wakishusha kwenye gari jeneza lenye mwili wa  askari mwenzao, marehemu Luteni Rajab Mlima wakati wa maziko yaliyofanyika jana katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam jana jioni Mlima ambaye alikuwa katika Jeshi la Umoja wa Mataifa la Kulinda Amani DRC Congo aliuawa akiwa kazini katika Mlima Gavana eneo la Goma.

   Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wakiwa wameinamia kwa huzuni  jeneza lenye mwili wa  askari mwenzao, marehemu Luteni Rajab Mlima wakati wa maziko yaliyofanyika jana katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam jioni hii. Mlima ambaye alikuwa katika Jeshi la Umoja wa Mataifa la Kulinda Amani DRC Congo aliuawa akiwa kazini katika Mlima Gavana eneo la Goma.
  Waombolezaji wakijiandaa kufanya maziko
 Waombolezaji wakifanya maziko
  Askari wa JWTZ wakitoa heshima wakati wa maziko
NA H@KI NGOWI
 
===
6
Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakifyatua risasi juu kama ishara ya heshima kwa marehemu Luteni Rajabu Ahmed Mlima katika shughuli za maziko kwa mujibu wa taratibu za Kijeshi.10
Meja Leonidas Benedict Luangisa akisoma wasifu wa marehemu. 11

====.
 
Hussein Makame, MAELEZO

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha ameongoza maziko ya marehemu Luteni Rajabu Ahmed Mlima aliyefariki dunia Oktoba 27 mwaka huu wakati akitekeleza jukumu la kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Marehemu Luteni Mlima alizikwa kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam saa 10 alasiri ambapo kabla ya hapo mwili wake ulipelekwa kwenye msikiti wa Maamur ukitokea nyumbani kwake Mbezi Beach na kisha kuswaliwa kabla ya kufikishwa kwenye makazi hayo ya milele.

Shughuli za maziko zilianza kwa waumini walioongozwa na Imamu wa msikiti wa Maamur, Ayoub Ali kuuweka mwili wa marehemu kwenye kaburi na kufuatiwa na dua na baadaye kuzikwa kwa mujibu wa utaratibu wa JWTZ kwa kupigiwa risasi baridi 4 hewani.

Akizungumza wasifu wa marehemu, Meja Leonidas Benedict Luangisa alisema kuwa marehemu alifariki dunia Oktoba 27 mwaka huu baada ya kupigwa risasi na waasi wa M23 eneo la Kiwanja mlima Gavana akilinda amani nchini DRC.

Naye Balozi Saleh Tambwe ambaye alitoa shukrani kwa kufanikisha mazishi ya jemadari huyo wa JWTZ alieleza kufarijika kutokana na Jeshi la DRC kutangaza kuukomboa mji wa Kiwanja ambao ndipo alipouawa marehemu Luteni Mlima.

Pamoja na Waziri Nahodha mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Juma Mwapachu.

Kwa mujibu wa Meja Luangisa marehemu Luteni Rajabu Ahmed Mlima alizaliwa tarehe 30 Agosti mwaka 1977 katika Kata ya Gongoni wilaya ya Taboro Mjini mkoani Tabora na kupata elimu ya Msingi katika shule ya msingi Mahenge.

Meja Luangisa alisema kuwa kuwa marehemu alipata Stashahada ya Juu ya Sayansi ya Kopmyuta katika Taasisi ya Usimamizi wa Fedha(IFM) mwka 2005 na kujiunga na Jeshi tarehe 7 Januari mwaka 2008, na baadae kutunukiwa Kamisheni ya Jeshi hilo..

Alisema kuwa katika utumishi wake Jeshini alifanikiwa kuhudhuria Kozi mbalimbali ikiwemo ya masuala ya Kinyuklia, Biolojia, na Kemia mwaka 2010 ambapo kabla ya hapo alipandishwa cheo kuwa Luteni Januari 10 mwaka 2009.

Kwa mujibu wa wasifu wake marehemu alifariki akiwa Kamanda wa Platuni Ulinzi wa Amani nchini DRC mwaka na vikosi vingine vya JWTZ nchini na kabla ya kifo chake marehemu alijaaliwa kupata mtoto mmoja.

Sote ni Wa Mwenyezi Mungu na Hakika sote tutarejea kwake, Mungu ailaze Roho ya Marehemu Luteni Rajabu Ahmed Mlima Mahali Pema Peponi, Amin.
NA FULL SHANGWE BLOG

0 comments:

Post a Comment