SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, October 15, 2013

Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbrod Ahitimisha Ziara Yake Ya Mafanikio Nchini Marekani

 Katibu Mkuu  wa Chadema Dr Wilbrod Slaa
Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbrod  Slaa akiangalia moja kati eneo lililotawanywa solar panel za kuzalisha umeme.Picha na Chadema

****
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na  Maendeleo ,Chadema Dr Wilbroad Slaa Jumapili 13 Oktoba amesafiri kurudi Tanzania baada ya Ziara yake iliyomchukua wiki tatu nchini Marekani. Dr Wilbroad Slaa aliwasili nchini Marekani tarehe 21 Septemba 2013 akiambatana na Mkewe mama Josephine Mushumbuzi na kupokelewa na Uongozi wa Chadema DMV. Tarehe 22 Septemba 2013 Dr Slaa alifanya mkutano uliojumuisha wanajumuia ya Watanzania waishio katika Majimbo ya Washington, Maryland na Virginia.
 
Katika ziara yake Dr Slaa alitembelea majimbo ya North Carolina na Alabama ambako alitembelea Vyuo Vikuu na Taasisi mbalimbali na kujifunza Shughuli nyingi za Maendeleo katika Sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo, Afya, Nishati na Uchumi.
 
Akizungumza akiwa uwanja wa Ndege wa Dulles mjini Washington Dr Slaa alisema alichojifunza akiwa Marekani anatarajia kupeleka maarifa hayo Tanzania ili yaweze kumkomboa Mtanzania kutoka katika Umaskini. Moja katika mambo ambayo amejifunza ni namna ya kutumia nishati ya Jua kuzalisha umeme hasa kwa wakazi wa Vijijini.
 
Dr Slaa amekamilisha ziara yake ya wiki tatu nchini Marekani iliyopewa jina la “Vision Tanzania” baada ya kualikwa na Umoja wa Vyuo vikuu nchini Marekani.

0 comments:

Post a Comment