SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, May 20, 2013

Kitimutimu cha Polisi na Wamachinga Iringa Jana, Mbunge wa iringa Mjini-Chadema Mch. Msigwa (Mb)Akamatwa

Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA)Picha juu amekamatwa na polisi jana hii kwa tuhuma kuwa ndiye chanzo cha kuhamasisha wafanya biashara wadogo wadogo (wamachinga) kufanya vurugu huko Iringa.Askari polisi wa kutuliza ghasia (FFU) katika Manispaa ya mji wa Iringa pia imewakamata zaidi ya watu hamsini, akiwemoo aliyekuwa mgombea udiwani katika kata ya Mvinjini, Abuu Majeck.

Biashara zilisimama wakati wa sekeseke hilo, moshi ulitanda kutokana na matairi kuchomwa moto katika barabara za kuu ya Iringa-Dodoma na ile ya Mashine Tatu. Jana  hii pia, Mbunge huyo alikuwa katika eneo la chuo cha Tumaini kwenye harambee iliyokuwa imehudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye kama inavyoonekana kwenye pichaa chini
 Mbunge Msigwa akisalimia katika harambee  iliyoendeshwa na  Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye(wa tatu Kushoto jana katika  chuo  cha Tumaini Iringa

 Mbunge wa iringa Mjini-Chadema Mchn Msigwa (kulia)akizungumza na msaidizi  wa askofu  wa KKKT dayosisi ya Iringa muda mfupi kabla ya kukamatwa na polisi jana

0 comments:

Post a Comment