SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, September 10, 2011

Taswira Za Uzinduzi Wa Kampeni Za Chadema igunga

Anaitwa Joseph Kashinye, Mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA jimbo la Igunga. "Ninashughulikia kupata mtandao wa uhakika. Leo siku haitoisha, nitakuwa nimepata suluhu la tatizo la Mtandao. Nitawaporomoshea kila kinachojiri huku. Asubuhi hii nimebahatisha kuingiza picha hiyo kwa taabu, imenichukua saa mbili kuingiza picha moja!  Pichani Kashindye alikuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa Igunga katika uzinduzi wa kampeni jana.
Mabango yenye ujumbe tofauti katika mkutano wa CHADEMA jana.
Katibu mkuu wa CHADEMA Dr Willbroad Slaa akihutubia mjini Igunga jana katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo jimboni hapa.Dr Slaaa alisema CCM hawana sababu ya kuchaguliwa kwa nafasi yoyote ile kwani kwa kipindi cha miaka 50 imeshindwa kumkomboa Mtanzania katika lindi la umaskini.Aliongeza kuseam kuwa CCM wanachokizinatia ni kutumia kila mbinu ili kushinda chaguzi na kushika dola ikiwa hawana malengo na mikakati madhubuti ya kumkomboa Mtanzania. Aliwaasa wana Igunga kumchagua Mgombea wa Chadema, Joseph Kashindye, ili awe mwakilishi wao kwani ni mtu makini anaetoka katika chama makini.
Mwenyekiti wa CHADEMA,Freeman Mbowe akihutubia maelfu ya wana Igunga jana katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za chaguzi mdogo jimboni la igunga.Mbowe alisema kuwa wana Igunga mungu amewapa bahati kubwa ya ufaya uchaguzi muda ,fupi  baada ya uchaguzi mkuu. Hivyo waitumie bahati hiyo wa kufanya mabadiliko. CCM haistaili kurudishwa tena madarakani jimboi hapa, kwani kuna masuala mengi ya msingi yanayohusiana na maendeleo ya wananchi CC imeshindwa kuyatekeleza kwa kipindi cha miaka 50.
Ilifika zamu ya Mgombea wa Ubunge jimboni hapa kwa Tiketi ya Chadema, Mwalimu, Mkaguzi wa Elimu, Joseph Lashindye.Kashindye alisema kuwa wana Igunga wtarajie mabadiliko ya haraka katika maendeleo.Yeye ameamua kwa makusudi kuacha ualimu na kuingia katika ulingO wa siasa. Amefanya kama Mwalimu Nyerere alivyofanya kwani Mwalimu Nyerere, aliaacha ualimu na kujiunga na TANU, matokea ya uamuzi huo wa mwalimu hakuna Mtanzania asiyeyaju.Na yeye alisema kuwa endapo wana-Igunga watamapa ridhaa ya kuwa mwakilishi atasimamia kwa nguvu zake zote misingi ya utu, uchapakazi na atahakikisha anaziba mianya yote ya rushwa katika halmashauri ya wilaya, ili fedha zinazotafunwa na wajanja, zifanye kazi iliyokusudiwa ya kuwaletea maendeleo wana- Igunga.
 Mbunge wa jimbo la Ubungo John Mnyika akiwahutubia wananchi wa jimbo la Igunga jana jioni katikauzinduzi wa kampeni za ubunge jimboni humo.

 Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini Mh. Joseph Mbilinyi akiwahutumia wakazi wa Igunga.
Kutoka kulia ni katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Wilbroad Slaa, Joseph Kashindye mgombea ubunge wa Jimbo la Igunga katikati na Mwenyekiti wa Chama hicho na mbunge wa jimbo la Hai wakielekea kwenye mkutano.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akihutubia maelfu ya wana Igunga jana katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za chaguzi mdogo jimboni la igunga.
Sehemu Kubwa ya Umati wa Wanachama Wa Chama Cha  Demokrasia na Maendeleo(Chadema)akielekea kwneye uzinduzi rasmi wa kampeni za Kuwania jimbo hilo.
 Mabango yalikuwa ni mengi lakini pia jeshi la polisi lilihakikisha kunakuwa na usalama wa kutosha. 
Picha na Mdau Victor Makinda na CHADEMA

0 comments:

Post a Comment