SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, August 12, 2010

Ahmadinejad na Abdullah wawapongeza Waislamu kwa kuanza mfungo wa Ramadhani

Sample Image
Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran pamoja na Mfalme Abdullah bin Abdulaziz wa Saudi Arabia wametoa mkono wa pongezi kwa wananchi wa nchi zao na Waislamu wote duniani kwa mnasaba wa kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani. Wakizungumza kwa njia ya simu viongozi hao pia wametoa wito kwa ulimwengu wa Kiislamu kuzidisha udugu na mshikamano hususan katika mwezi huu wa toba na baraka. Rais Ahmadinejad amewaomba Waislamu kote duniani kujikurubisha zaidi kwa Mwenyezi Mungu kwa kukithirisha ibada. Kwa upande wake Mfalme Abdullah amesema huu ni mwezi wa mavuno ya thawabu na kwa mantiki hiyo Waislamu wanapaswa kutumia fursa hiyo barabara. Inafaa kukumbusha hapa kuwa ibada ya Saumu ni nguzo ya nne ya Uislamu na kila Muislamu analazimika kutekeleza ibada hiyo isipokuwa wale walio na sababu zinazokubalika kisheria.

0 comments:

Post a Comment