SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, August 12, 2010

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran: Nchi za Magharibi zitajuta

 Sample Image

Manouchehr Muttaki Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, nchi za Magharibi zitajuta. Akizungumzia vikwazo vya upande mmoja visivyokuwa vya kiadilifu vya Marekani na Umoja wa Ulaya dhidi ya wananchi wa Iran, Muttaki amesisitiza kuwa, nchi za Magharibi zitakuja kujuta kutokana na nyendo zao zisizokuwa za kisheria na kimantiki kama ilivyotokea miaka iliyopita. Amesema kuwa, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Umoja wa Ulaya ulichukua misimamo kama hiyo ya kijuba dhidi ya Iran, na kupelekea Tehran kuimarisha mashirikiano yake na nchi za maeneo mengine. Akizungumzia vitisho vinavyotolewa mara kwa mara na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Manouchehr Muttaki amesema kuwa, utawala wa Israel na Marekani zinaelewa wazi kwamba, kama zitaanzisha vita dhidi ya Iran, basi nhci hizo hazitakuwa na uwezo wa aina yoyote wa kusimamisha vita hivyo. 

0 comments:

Post a Comment