Yussuf Ahmed Alley AKA Bwan Chuchu amefariki dunia jijini Nairobi-Kenya. Chuchu alijipatia umaarufu mkubwa miaka ya mwanzoni mwa 2000 na bendi yake ya Chuchu Sound,iliyokua na wakali kama Mao Santiago,Omary Mkali,Waziri Sonyo,marehemu Gabby Katanga na wengine kibao,hasa na kibwagizo cha ''EEH..KWAHERI'' kwenye miondoko ya mduara. Na mpaka anafariki alikua anamiliki studio ya Heartbeat Records na kituo cha redio cha Chuchu FM vyote vipo kisiwani Zanzibar,na haijajulikana mara moja chanzo cha kifo chake. Msiba upo Kisima Majongoo na Mazishi yanafanyika kwenye makaburi ya MwanaKwerekwe leo saa 10,kisiwani Zanzibar.
MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI...AMIN!
Hali
ndivyo ilikuwa kama unavyoona picha hiyo hao ni baadhi ya watu
waliojitokeza kuusindikiza mwili wa Marehe Yussuf Alley Almaarufu
Bwanchuchu
Mamia ya wananchi na wasanii nchini jioni hii wanahudhuria mazishi
ya msanii maarufu wa Zanzibar Yusuf Ahmed Alley maarufu bwan’chuchu
katika makaburi ya Mwanakwerekwe wilaya ya magharibi.
Kusikia kimoja ya vibao vya Chuchu Sound BOFYA
HAPA
HATIMAE CHUCHU AZIKWA LEO
Hali
ndivyo ilikuwa kama unavyoona picha hiyo hao ni baadhi ya watu
waliojitokeza kuusindikiza mwili wa Marehe Yussuf Alley Almaarufu
BwanchuchuKwa mujibu wa chanzo chetu cha habari Marehemu Chuchu amefariki dunia mjini Nairobi, Kenya alikopelekwa kupatiwa matibabu baada ya kuugua kiasi ya mwezi mmoja uliopita.
Mwili wa msanii umerejeshwa mjini hapa ambapo taratibu za mazishi zilifanyika katika mtaa wa Kisima Majongoo na maziko yanafanyika jioni hii katika makaburi ya Mwanakwerekwe wilaya ya magharibi.
24 SEVEN 365 INATOA MKONO WA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU.





0 comments:
Post a Comment