SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, May 17, 2010

Hali nchini Rwanda

Matumizi ya nguvu yanazidi miezi mitatu kabla ya uchaguzi wa rais nchini Rwanda


Mtu mmoja ameuwawa na wengine 28 kujeruhiwa jana usiku baada ya bomu la mkono kufyetuliwa katika mtaa wa kibiashara wa mji mkuu wa Rwanda-Nyabugogo,mjini Kigali.
Hilo ni shambulio la tatu katika kipindi cha miezi mitatu kufanywa katika eneo hilo hilo linalotembelewa na watu wengi mjini Kigali.
Mashambulio matatu yameshatokea,tangu february 19 katika eneo hilo linalolindwa vikali na vikosi vya usalama nchini Rwanda.Jumla ya watu watatu wamepoteza maisha yao na wengine wasiopungua 50 kujeruhiwa.Hakuna aliyedai kuhusika na mashambulio hayo.Polisi wameahidi kuwasaka na kuwakamata wahusika.
Mashambulio haya yanatokea katika wakati ambapo Rwanda inajiandaa kuitisha uchaguzi wa rais Agosti tisaa mwaka huu.Rais Paul Kagame ameshachaguliwa na chama chake cha Patriotic Front kutetea wadhifa wake.
Mandishi :Hamidou Oummilkheir

0 comments:

Post a Comment