SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, July 7, 2014

BANDA LA BENKI KUU LAWAVUTIA WENGI KWENYE MAONYESHO YA SABASABA

 Wadau wakiendelea kumiminika kwa wingi kwenye Banda la Benki Kuu lililopo kwenye Viwanja vya Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (Sabasaba).
 Mmoja wa Maafisa wa Benki Kuu akitoa maelezo kwa Wadau waliotembelea kwenye Banda hilo ili kufahamu maswala mbali mbali ya Kibenki,wakati wa Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
 Maafisa wa Benki Kuu wakiendelea kutoa somo wa watu mbali mbali waliofika kwenye banda hilo,huku moja wa somo ni lile la kuweza kutambua na kutofautisha noti bandia na noti halali.
 Benki kuu yatoa sarafu ya jero (mia tano) kama ionekanavyo pichani,ila bado haijaingia mtaani mpaka hapo itakapotangazwa kuanza kwa matumizi yake.
 Ndani ya Banda hilo kuna sehemu ya kubadili noti chakavu na ukapata mpya. 
 Picha za Magavana wa Benki Kuu toka wa kwanza mpaka wa sasa.
 Wadau wakiendelea kupatia taarifa za kibenki. 
 Sehemu ya Mapokezi.
 Taswira ya ndani katika muonekano wa jicho la samaki.
Timu nzima ya wafanyakazi wa Benki Kuu waliopo kwenye Maonyesho ya Sabasaba wakiwa kwenye picha ya pamoja.

0 comments:

Post a Comment