SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, March 17, 2014

BUNGE LA KATIBA LASITISHWA KWA MUDA BAADA YA ZOMEA ZOMEA YA WAJUMBE

Shughuli za Bunge Maalum la Katiba zimeshindwa kuendelea jioni hii ambapo Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba alitakiwa kuwasilisha Rasimu ya Katiba kwenye Bunge hilo.
Kabla hajaanza, wajumbe walianza kuzomea wengine wakipiga kelele ndipo Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge hilo, Samuel Sitta alipoamua kusitisha shughuli za bunge mpaka itakapotangazwa.