SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, March 19, 2014

BOL MKOMBOZI WA WATUMIAJI WA SIMU NCHINI HAPA NCHINI

Afisa Mtendaji Mkuu wa BOL, Afrika Mashariki, Abdullatif Bouziani, akizungumza kwenye uzinduzi huo.

…Akizindua rasmi huduma hizo.
Wanahabari wakishuhudia uzinduzi huo.
Balozi wa kampuni hiyo hapa nchini ‘Mkwere Orijino’ (katikati) Abdullatif na kulia ni Afisa Masoko wa kampuni hiyo Afrika Mashariki, Brian Azemchap wakiwa kwenye pozi la furaha baada ya uzinduzi.
Afisa Mtendaji wa kampuni hiyo akijibu maswali ya wanahabari.
Wafanyakazi wa kampuni hiyo wakiwasajili wateja wa mtandao huo (hawapo pichani).
Kampuni za simu nchini zimezidi kupata changamoto baada ya kampuni mpya ya BOL Smart ‘Lets Talk' kuzindua huduma zake hapa nchini ambazo zinaungana katika mtandao wa pamoja wa nchini za Afrika Mashariki, Uganda, Burundi, Tanzania.
Akizungumza na wanahabari kwenye mkutano na wanahabari uliofanyika Serena Hoteli jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo Afrika Mashariki, Abdullatif Bouziani, aliwataka wananchi kutumia mtandao huo wa gharama nafuu kuliko yote hapa nchini na hivyo kuwakomboa watumiaji wa simu. Mteja wa mtandao huo atatozwa shilingi 79 kila atakapopiga simu na kuzungumza kwa dakika zozote anazotaka.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL)