SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, September 30, 2010

Benki kuu ya Kenya kuchunguza "Hawala"
Kenya imetangaza mipango inayonuia kudhibiti ufadhili wa kifedha unaotolewa kwa wapiganaji wa kiisilamu wa Al- Shabaab nchini Somalia.
Benki Kuu ya Kenya imeziagiza benki zote nchini kuchunguza shughuli za kibiashara zinazohusishwa na wafanyibiashara walioorodheshwa kama wafadhili wa ugaidi na Umoja wa Mataifa.
Hatua ya Kenya katika kujaribu, kupunguza nguvu za wanamgambo wa Ki-Somali inatokea wiki moja baada ya baraza la usalama la umoja wa Mataifa kufanya kikao maalum kilichoangazia hali ya Somalia.
Wadadisi wa mambo ya usalama wamekuwa wakisisitiza kwamba Nairobi imekuwa kivukishio cha ufadhili wa makundi yanayokabiliana na serikali ya mpito ya somalia.
Moja ya njia zinazotumiwa na wasomali kuwatumia jamaa zao fedha ni Hawala.

0 comments:

Post a Comment