SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, August 19, 2010

Mambo yalivyokuwa katika Mtanange wa Simba naYanga



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Leodger Tenga (kulia) akimkabidhi Nahodha wa timu ya Yanga, Freddy Mbuna Ngao ya hisana baada ya kuwafunga watani wao wa jadi Simba kwa mikwaju ya penati 3-1 baada ya kutoshana nguvu kwa dakika 90 wakati wa mchezo huo wa kuwania Ngao ya Hisani uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Wachezaji na Viongozi wa Yanga, wakipozi na Ngao yao ya hisani baada ya kukabidhiwa kwa kuwatungua watani wao wa jadi.Beki wa Simba Juma Jabu (kulia) akilala kuokoa krosi iliyokuwa ikipigwa na beki wa yanga, Isack Baokye, wakati wa mchezo huo.
Beki wa Simba, Joseph Owino (kushoto) akimvuta jezi Keneth Asamoh, baada ya kulambwa chenga, wakati wa mchezo wa kuwania Ngao ya Hisani uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Nsa Job wa Yanga (namba 24 mgongoni) akiruka kukwepa kwanja la beki wa Simba, Juma Nyoso.
Golikipa wa Yanga, Yaw Berko akiokoa mchomo wa kwanza wa Simba wakati wa hatua ya penati.
Uhuru Seleman, akishika kichwa kujilaumu kwa kukosa penati
Wachezaji na mashabiki wa Yanga, wakishangilia ushindi
Muandishi: Othman Michuzi |

0 comments:

Post a Comment