SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, August 19, 2010

MAHOJIANO NA ISSA MICHUZI JUU YA UJIO WA MICHUZIPOST.COM
Upende,usipende,leo hii unapoongelea masuala ya nyanja ya habari na mawasiliano kupitia zana za blog kwa upande wa Tanzania(Tanzanian Blogsphere), huwezi kuepuka kumtaja Muhidin Issa Michuzi a.k.a Ankal,Mzee wa Libeneke.
Mwanzoni alipoanzisha blog yake maudhui yake yalikuwa zaidi ni picha na maelezo kidogo juu ya picha hiyo au picha hizo.Hiyo ilitokana na ukweli kwamba Michuzi ni seasoned professional photographer.
Baada ya muda fulani,na kutokana na mafanikio aliyokuwa ameyapata,ilimlazimu kutanua wigo wa blog yake na hivyo kutoishia katika picha na maelezo mafupi mafupi tu bali kujumuisha maelezo au habari zaidi.Leo hii,blog yake imekuwa kimbilio la wengi pale wanapotafuta habari motomoto kuhusu kinachoendelea nchini Tanzania,maeneo ya jirani na hata sehemu mbalimbali za ulimwengu.
Hivi sasa yupo mbioni(keshazianza mbio zenyewe) kuboresha zaidi kazi ngumu anayoifanya ya kuendeleza “libeneke”.Ameanzisha tovuti/blog mpya inayopatikana kupitia http://michuzipost.com
BC imepata nafasi ya kuongea naye machache kuhusu ujio huo wa MichuziPost na mambo mengine kuhusiana na tasnia ya habari na mawasiliano. Je,”wadau” watarajie nini katika uwanja huo mpya?Nini siri ya mafanikio yake mpaka hivi sasa?Ana ushauri gani kwa bloggers wapya na wale wanaofikiria kuanzisha blog?Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;
BC: Kwanza nikupe Hongera nyingi kwa kazi nzito unayoifanya.Mambo yanakwendaje?
MICHUZI: Ahsante sana, mambo mswano tu. Libeneke kwa kwenda mbele. Yaani baada ya miaka mitano ya tufanikio kiduchu tulikopatikana, sasa ni wakati muafaka wa kupiga hatua tano mbele, na kusaidia ujenzi wa taifa letu kwa njia ya habari.
Nitakuwa mtovu wa hisani na fadhila endapo kama nitaanza kujieleza bila kwanza kuwashukuru wadau wa Globu ya Jamii popote walipo duniani, kwani bila sapoti yao sidhani kama ningefikia robo tu ya hapa nilipo.
Naomba kwa heshima na taadhima wape AHSANTE SANA wadau. Waambie nawapenda, nawaheshimu na nitandelea kuwa mtumishi wao wakati wa raha na wakati wa shida. Pia naomba ninaowaudhi kwa njia moja ama nyingine wanisamehe kwani mie ni binadamu na si kamilifu. Pia si rahisi kumridhisha kila mdau kwa kila jambo. Napenda sana kutumia ule msemo wa ‘what’s good for the goose, is bad for the hen’. Hivyo naomba uvumilivu na kuelekezana pale palipo na dosari.
habari zaidi bofya hapa: http://bongocelebrity.com/

0 comments:

Post a Comment