SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, July 14, 2010

Mwanasayansi Muirani aliyetekwa nyara na Marekani aelekea nyumbani
Sample ImageMwanasayansi Muirani Shahram Amiri ambaye alitekwa nyara na mashirika ya kijasusi ya Marekani na Saudi Arabia mwaka jana ameondoka Marekani akielekea Tehran, mji mkuu wa Iran.
Msomi huyo Muirani alikimbilia hifadhi katika Kitengo cha Maslahi ya Iran katika Ubalozi wa Pakistan mjini Washington Jumanne na kuomba arejeshwe Iran mara moja. Ubalozi wa Pakistan unalinda maslahi ya Iran huko Marekani kwa sababu nchi hizi mbili hazina uhusiano wa kidiplomasia. Majasusi wa Marekani wakishirikiana na wenzao wa Saudia walimteka nyara Amiri alipokuwa katika ibada ya Umra nchini Saudi Arabia mwezi Juni 2009 na baada ya kutekwa nyara alipelekwa Marekani. Katika mikanda ya video aliyotoa, Amiri alisema alitekwa nyara na majasusi wa Marekani wakishirikiana na kikosi cha kijasusi cha Saudia kijulikanacho kama Istikhbarat mjini Madina. Wadadisi wa Mambo wanasema mashirika ya kijasusi ya Marekani yameamua kumuachilia huru Amiri baada ya kushindwa kumtumia katika propaganda zao dhidi ya mpango wa nyuklia wa Iran. Amiri amesema aliteswa sana alipokuwa mikononi mwa makachero wa Marekani.
http://kiswahili.irib.ir
**********************
Mwili wa makamu wa rais wa chama cha upinzani nchini Rwanda wapatikana 
Mwili huo wa Andre Kagwa Rwisereka umepatikana karibu na gari lake lililokuwa limetelekezwa.
Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Mwili wa Makamu wa Rais wa chama cha upinzani ambacho hakijasajiliwa nchini Rwanda cha Democratic Green, Andre Kagwa Rwisereka, hatimae umepatikana karibu na gari lake. Rwisereka alikuwa hajulikani alipo baada ya gari lake kukutwa limetelekezwa karibu na mji wa Butare. Haya yametokea wakati kukisalia wiki chache kabla ya uchaguzi wa rais nchini humo mwezi ujao.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi pamoja na chama cha Democratic Green imethibitisha kupatikana kwa mwili wa Bwana Rwisereka aliyetangazwa kutojulikana alipo mapema jana. Gari la makamu huyo wa rais wa chama hicho cha upinzani lilikutwa karibu na mto Mukula mjini Butare. Msemaji wa polisi Eric Kayiranga amesema mwili wa Bwana Rwisereka umepatikana majira ya asubuhi ya leo umbali wa kilometa tatu kutoka eneo ambako gari lake lilionekana, huku kukiwa na kisu kikubwa kinachodhaniwa ndicho kilitumika katika mauaji yake. Kayiranga amesema watu waliomuona usiku kabla ya kutoweka wamesema alikuwa na fedha nyingi, hivyo wanahisi huenda lilikuwa ni tukio la ujambazi na kwamba uchunguzi wa tukio hilo tayari umeshaanza. Msemaji huyo wa polisi amesema mwili huo umekutwa ukiwa na majeraha kifuani na umepelekwa hospitali.
Bwana Habineza amesema chanzo cha mauaji hayo bado hakijajulikana na kwamba sasa na yeye anaishi kwa woga kwa sababu hapo awali alishawahi kupokea vitisho kutoka kwa watu wasiojulikana. Chama cha Democratic Green kimekuwa kikishindwa kupata usajili utakaokiwezesha kushiriki katika uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika mwezi ujao. Kwa upande mwingine mashirika ya kutetea haki za binaadamu yameilaumu serikali ya Rwanda kwa kukandamiza wapinzani pamoja na vyombo vya habari kuelekea kwenye uchaguzi huo. Aidha, Rwanda imekanusha tuhuma hizo ikisema kuwa serikali imekuwa ikifanya mazungumzo na kukubaliana na baadhi ya maoni ya wapinzani tangu yalipotokea mauaji ya kimbari mwaka 1994.
Hata hivyo, polisi nchini Rwanda wamemkamata mwandishi habari wa kujitegemea kwa tuhuma za kumfananisha Rais Paul Kagame na kiongozi wa Manazi a Ujerumani, Adolf Hitler. Polisi imelithibitisha hilo, ingawa afisa wa polisi amekanusha kuwa kukamatwa kwake kunahusiana na uchaguzi mkuu ujao. Msemaji wa polisi nchini Rwanda, Eric Kayiranga alisema kuwa Saidati Mukabibi, mwandishi wa gazeti la kujitegemea la Umurabyo alikamatwa kwa kosa la kukashifu, kuvuruga usalama wa nchi na ubaguzi wa kikabila. Baraza la habari la Rwanda-MHC limesema kukamatwa kwa Mukabibi hakuhusiani na uchaguzi ujao, ambao Rais Kagame anategemewa kushinda kwa kupata wingi wa kura.
Mwandishi: Grace Patricia Kabogo (RTRE)

0 comments:

Post a Comment