SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, June 28, 2010

England yachapwa na Ujerumani 4-1

Miroslav Klose akipongezwa na wenzie baada ya kuandika goli la kwanza la Ujerumani.
engine mawili yalifungwa na Thomas Mueller katika kipindi cha pili.Washabiki wa
 timu ya taifa ya soka ya Ujerumani, wakishangilia timu yao, ilipoinyuka
 Uingereza goli nne kwa moja, hapo jana, nchini Afrika kusini. 
Washabiki wa timu ya taifa ya soka ya Ujerumani, wakishangilia timu yao, ilipoinyuka Uingereza goli nne kwa moja, hapo jana, nchini Afrika kusini.
Ujerumani imefuzu kucheza robo fainali ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini, baada ya kuifunga England mabao 4-1 katika uwanja wa Free State mjini Bloemfontein.
Mechi hiyo ambayo England walionyesha kulemewa katika safu ya ulinzi, pia itakumbukwa kwa kukataliwa bao la wazi lililofungwa katika dakika ya 38 na Frank Lampard.
Ujerumani walitangulia kufunga katika dakika ya 20 kupitia Miroslav Klose, na katika dakika ya 32 Lukas Podolski akaongeza goli la pili.
Katika dakika ya 37, England walipata kona na mlinzi Mathew Upson akafunga kwa kichwa kuipatia England goli pekee. Dakika moja tu baada ya bao hilo Frank Lampard alipiga mpira wa mbali ambao uligonga juu ya mwamba kabla ya kudunda ndani ya goli la Ujerumani.
Utata
Lakini mwamuzi Uruguay Jorge Larrionda kutoka Uruguay alifuata ushauri wa msaidizi wake wa pembeni na kuendeleza mchezo bila kutambua bao hilo.
Kipindi cha pili kilimalizika Ujerumani wakiongoza 2-1, na majaribio kadhaa ya mashambulizi ya England hayakufanikiwa.
Thomas Mueller alizamisha kabisa matumaini ya England kwa kufunga mabao mawili katika kipindi cha dakika tatu, moja katika dakika ya 67 na la nne katika dakika ya 70.
Kocha wa Ujerumani, Joachim Loew, akiwa ameshapata imani ya ushindi alifanya mabadiliko yaliyoonekana ya kuwapumzisha washambuliaji muhimu kwa ajili ya robo fainali.
Meneja wa England, Fabio Capello, pia alifanya mabadiliko kadhaa katika kipindi cha pili kuimarisha ushambuliaji lakini bila mafanikio.

TAZAMA VIMBWANGA VYA PWEZA ALIYETABIRI USHINDI WA GERMANY DHIDI YA ENGLAND
 

0 comments:

Post a Comment