SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, June 22, 2010

Mshukiwa wa shambulizi akiri makosa Marekani

Mshukiwa wa njama ya kulipua bomu katika eneo la Times Square nchini Marekani
    Mtu anayedaiwa kupanga njama ya kulipua bomu lililotegwa ndani ya gari katika bustani la Times Square mjini New York Marekani, mwezi May, amekiri mashtaka yote kumi dhidi yake.
   Faisal Shahzad raia wa Pakistan, amekiri kumiliki zana zenye maangamizi makubwa akiwa na nia ya kutumia katika njama yake iliyotibuka.
   Shahzad aliyekamatwa siku mbili baada ya shambulizi hilo wakati akijaribu kuondoka nchini humo kuelekea Dubai, alikiri kugeza gari lake lililokuwa na bomu karibu na eneo la Times Square jumamosi jioni.
   Bomu hilo lilipatikana baadaye huku stakabadhi za mahakamani zikidai kuwa bwan Shazhad alipokea pesa pamoja na mafunzo kuhusu namna ya kulipua mabomu kutoka kwa kundi la Taleban nchini Pakistan.
   Hata hivyo alisema yuko tayari kukiri makosa hayo kuonyesha kuwa Marekani ingali inakabiliwa na tisho la mashambulizi zaidi ikiwa hawatondoka nchini Afghanistan na Iraq.

Ajali ya ndege msituni Congo

Ramani ya Congo
  Maafisa wakuu nchini Congo wamethibitisha kutokuwepo manusura wa ajali ya ndege iliyotokea kati ya msitu wa Congo Brazaville na Cameroun siku ya Jumanmosi.
Ndege hiyo ilikuwa imewabeba wakurugenzi ya makampuni ya madini wengi wakiwa raia wa Australia.
Watu hao akiwemo mfanyabishara na tajiri mkubwa nchini Australia, Ken Talbot walikuwa safarini kutoka Cameroun kuzuru mgodi wa chuma, nchini Congo.
Takriban Maiti wote walipataikana, ingawa waziri wa mambo ya nje wa Australia,itachukua muda kabla ya kuwatambua na kisha kuwarejesha nyumbani maiti.
Kiini cha ajali kingali kujulikana.
bbc swahili

0 comments:

Post a Comment