
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiangalia kazi za uchoraji zinazofanywa na watu wenye ulemavu wa ubongo wanaolelewa katika kituo Kharafi Kids Activity Center wakati Mama Salma alipotembelea kituoni hapo tarehe 6.5.2013.
Na Anna Nkinda – Kuwait
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amekiomba kituo cha watoto wenye mtindio wa Ubongo kilichopo nchini Kuwait kushirikina na Tanzania ili waweze kufanya kazi kwa pamoja ya kuwasaidia na kutoa mafunzo kwa watoto wenye matatizo kama hayo waliopo nchini.
Mama Kikwete ametoa ombi hilo alipotembelea kituo hicho kwa ajili ya kuona jinsi wanavyotoa mafunzo kwa watoto hao ambayo yameweza kuwabadilisha akili zao na kuwa sawa na za watu wengine.



