Liverpool imekubali kumuuza mshambulizi wake Luis Suarez kwa Barcelona kwa kima cha pauni milioni 75.
Mchezaji huyo wa Uruguay mwenye umri wa miaka ,
27, ambaye amepigwa marufuku ya miezi miinne kwa kumuuma mchezaji
mwenzake wa Italy, Giorgio Chiellini wakati wa mechi yao katika kombe la
dunia, atasaini mkataba wa miaka mitano.



