
Na Mwandishi Wetu, Johannesburg
Kwa hisani ya http://www.salehjembe.blogspot.com/
Kiungo Mshambuliaji wa Free State
Stars, Mrisho Ngassa naye amejiunga na kikosi cha Taifa Stars kilicho
mazoezini jijini Johannesburg.
Ngassa alichelewa kujiunga na kambi hiyo kwa kuwa alikuwa akiichezea timu yake katika mechi ya Ligi Kuu frika Kusini.
Ngassa amejiunga na wenzake na mara moja ameanza mazoezi akiwa na kikosi cha Stars kinachojiandaa kucheza na Algeria
Stars itaivaa Algeria kuwania kucheza Kombe la Dunia katika mechi inayotarajiwa kuwa ngumu.
0 comments:
Post a Comment