SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, November 2, 2015

AZAM FC YAIFUNGA TOTO AFRICAN 5-0

 Mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu akitafuta mbinu za kumtoka veki wa Toto African,  Hamis Seleman katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. (Picha na Francis Dande)

Beki wa Toto African, Salum Chuku (katikati) akichuana na mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu (wa pili kushoto) wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Chamazi jijini Dar es Salaam jana. Azam ilishinda 5-0. 
 Kipre Tchetche akimiliki mpira huku beki wa Toto African akijaribu kumzuia.
Wachezaji wa Azam FC wakishangilia baada ya kupata bao.
 Kocha Mkuu wa Toto African, Martin Grelics (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na kikosi cha kwanza cha timu hiyo kilichoanza kucheza na Azam FC kwenye Uwanja wa Chamazi. Kocha huyo amevunja mkataba na kuwaaga wachezaji wa timu hiyo.
Wachezaji wa Toto African  wakiwa wamebeba ujumbe uliokuwa unasomeka 'Asante Sana Kocha Martin' 
 Kocha Mkuu wa Toto African, Martin Grelics akiagana na wachezaji wake baada ya mchezo na Azam FC kwenye Uwanja wa Chamazi. Kocha amevunja mkataba na timu hiyo.
 Wachezaji wa Toto African wakiomba dua katika mchezo wao dhidi ya Azam FC.

0 comments:

Post a Comment