SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, November 17, 2014

WAFUGAJI WAVAMIA ENEO LA MWEKEZAJI NA KUCHOMA NYUMBA ,MAGARI


Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Siha ,Rashid Kitambulilo akimuongoza mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama wakati akitembelea eneo la mwekezaji la Tanganyika Film and Safari ambako wafugaji jamii ya Masai wanadaiwa kufanya uharibifu mkubwa.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama pamoja na kamati ya ulinzi na usalama wakitizama uharibifu  uliofanywa na wafugaji jamii ya Masai.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akitizama moja ya gari lililochomwa moto na watu wanaodaiwa kuwa ni wafugaji jamii ya Masai.
Uharibifu mkubwa umefanyika ambapo nyumba 16 na magari tisa yameteketea moto.
Mwekezaji Peter Jones akizungumza na wanahabari kuhusu tukio hilo lililomsababishia hasara kubwa.

0 comments:

Post a Comment