SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, November 16, 2014

Bonanza la Ufunguzi wa Wiki ya Mlipa Kodi ya TRA lafanyika leo jijini Dar

Kaimu Mkurugeni wa Elimu na Huduma wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Allan Kiulla (kulia) akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kwenye Bonanza la Ufunguzi wa Wiki ya Mlipa Kodi lililofanyika leo kwenye viwanja vya TCC Club,Chang'ombe jijini Dar es Salaam.Bonanza hilo lililogeshwa kufanyika michezo mbali mbali,ikiwepo mpira wa miguu,mpira wa pete,kuvuta kamba na mingine mingi.Wa pili kulia ni Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki ambaye ndie alikuwa Mgeni Rasmi kwenye Bonanza hilo.Picha zote na Othman Michuzi.
CREDIT TO MICHUZI MATUKIO BLOG

Mgeni rasmi kwenye Bonanza la Ufunguzi wa Wiki ya Mlipa Kodi ambaye ni Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki akitoa nasaha zake kwa washiriki wa Bonanza hilo lililofanyika leo Novemba 15,2014 kwenye viwanja vya TCC Club,Chang'ombe jijini Dar es Salaam.



Sehemu ya Wafanyakazi wa  Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wafanyakazi wa NSSF ambao ni Waalikwa walioshiriki kwenye Bonanza la Ufunguzi wa Wiki ya Mlipa Kodi wakifatilia kwa makini nasaha za Mgeni Rasmi,ambapo kauli mbiu ya Mwaka huu ni "Risiti ni Haki Yako,Unaponunu Dai Risiti na Unapouza ni Lazima Utoe Risiti".
Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Tiagi Masamaki akifatilia kwa makini michezo mbali mbali iliyokuwa ikiendelea uwanjani hapo.
MC wa Bonanza akiendelea na Wajibu wake.
Mtanange wa kukata na shoka kati ya Timu ya TRA na timu ya NSSF ulipigwa katika Uwanja wa TCC Chang'ombe,Mtanange uliowatoa kifua Mbele vijana wa NSSF kwa Mabao 4-2 dhidi ya wenzao wa TRA.
Hatari langoni mwa timu ya NSSF paleeeeeee.........
Beki wa Timu ya TRA akijaribu kumdhibiti Mshambuliaji wa timu ya NSSF katika Mtanange uliopiga leo kwenye viwanja vya TCC Club Chang'ombe,jijini Dar es Salaam.Hadi mwisho wa Mchezo,NSSF ilishinda 4  - 2  dhidi ya TRA.
Holaaaa.....
Anakataa paleee Beki wa TRA.
Hapiti mtu hapaaaaa.........
Mashabiki wa timu ya NSSF wakiishangilia timu yao baada ya kuibuka kidedea kwa kuichapa timu ya TRA Bao 4-2.
Kiongozi wa Kundi la Ngoma za Asili,Wanne Star akiipanga vyema timu yake wakati wa kutoa burudani uwanjani hapo.
Vijana wa Kundi la Wanne Star wakionyesha makeke yao mbele ya wadau wa TRA waliofurika kwa wingi kwenye viwanja vya TCC Club,Chang'ombe jijini Dar es Salaam leo.
Dada Oliver wa TRA akiongoza shughuli hiyo.
Nyoka wa Wanne Star kachachamaa na hataki zereuuuu..........
Yalaaaaaaahhh......
Taswira za wadau mbali mbali wa TRA wakiwa wamembeba Nyoka wa Wanne Star.














































Team nzima ya Michuzi Media Grop katika picha ya pamoja.

0 comments:

Post a Comment