SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, March 21, 2014

NJIA MPYA YA USAFIRISHAJI WA MADAWA YA KULEVYA ILIYOGUNDULIWA BAADA YA KUWANASA WANAIGERIA NA MTANZANIA MMOJA

Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu Dar es Salam, Suleiman Kova alitaja majina ya Wanaijeria hao kuwa ni Sunday Chaidikaobi (42), Chukwuma Favour (31), na Franklin Indubuisi (41). Mtanzania aliyebambwa pamoja na Wanaijeria hao ametajwa kuwa ni bi Hadija Ngoma (43), mkazi wa Kimara Temboni, Dar es Salaam.
RAIA watatu wa Nigeria na mwanamke wa Kitanzania wamekamatwa na polisi jijini Dar es Salaam, wakituhumiwa kujaribu kusafirisha madawa ya kulevya kwenda nchini Liberia. Watuhumiwa hao wanadaiwa kuwa walikuwa mbioni kutuma mihadarahi hiyo, ikiwa kwenye vitabu, kwa kutumia Wakala wa Usafirishaji Mizigo ya DHL.
Kwa mujibu wa Kamanda Kova, polisi walipata taarifa juzi, Machi 18, kuwa kuna watu wanne wanajihusisha na usafirishaji wa dawa za kulevya waliokuwa katika ofisi za DHL zilizopo Barabara ya Sam Nujoma.
Kufuatia taarifa hizo, Kamanda Kova amesema “makachero walifuatilia suala hilo na hatimaye siku hiyo saa 8:30 mchana watu hao walikamatwa wakiwa na kifurushi wakijiandaa kukisafirisha kwenda nchini Liberia.”
Alisema polisi walipopekua kifurushi hicho, walikuta vitabu vitatu vya Kiingereza. Walipopekua vitabu hivyo, walikuta madawa aina ya heroin katika kurasa za mwanzo.
“Katika vile vitabu kurasa ya kwanza inayofunika lile jalada gumu kwa ndani, walikuwa wamefunua na kuweka unga huo na katika ukurasa wa nyuma vivyo hivyo kwa vitabu vyote,”aliongeza.
Unga huo unaokadiriwa kuwa na uzito wa nusu kilo, umepelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali kwa uchunguzi zaidi kubaini thamani na uthibitisho wa madawa hayo.
 Miezi kadhaa iliyopita, Wanigeria wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta nchini Kenya, wakijaribu kusafirisha dawa za kulevya aina ya cocaine zenye thamani ya takriban shilingi milioni 120;